Mahakama yaombwa imuonye wakili wa Masogange ...soma habari kamili na matukio 360...#share
Na
Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
UPANDE
wa mashtaka katika kesi ya kutumia dawa za kulevya inayomkabili, Agnes Gerald ‘Masogange’ umeitaka mahakama ya hakimu mkazi Kisutu kuuonya upande wa utetezi kuchelewesha kesi hiyo.
Agnes Gerald 'Masogange' aliyevaa miwani.
Ombi
hilo limetolewa na upande wa mashtaka kutokana na upande wa utetezi kushindwa
kutoa ushahidi wao kwa mara ya tatu mfululizo.
Hatua
hiyo imekuja baada ya Wakili wa utetezi, Nehemia Nkoko kudai mbele ya Hakimu
Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri kuwa Wakili mwenzake anayemtetea Mshtakiwa
Msogange, Reuben Simwanza, ndiye aliyeandaa mashahidi lakini ameshindwa kufika
kwa kuwa anaumwa.
Nkoko
amongeza, atahakikisha anaandaa mashahidi ili ikitokea wakili mmoja wao hayupo,
mwengine aendelee na kesi.
Wakili wa Serikali, Constantine Kakula alidai kuwa hawana pingamizi na sababu zilizotolewa na upande wa utetezi lakini wanaomba mahakama itambue kuwa ni mara ya tatu kesi kwa upande wa utetezi inaahirishwa.
Wakili wa Serikali, Constantine Kakula alidai kuwa hawana pingamizi na sababu zilizotolewa na upande wa utetezi lakini wanaomba mahakama itambue kuwa ni mara ya tatu kesi kwa upande wa utetezi inaahirishwa.
"Mawakili
wapo wengi lakini wanashindwa kuendelea kutoa ushahidi wao wa upande wa utetezi
basi kama hawawezi, waache mshitakiwa aendelee na kesi mwenyewe," alidai
Kakula.
Pia aliiomba mahakama kutoa ahirisho la mwisho kwa sababu kesi ni ya muda mrefu. Kutokana na hali hiyo, Hakimu Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 26, mwaka huu kwa ajili ya kusikilizwa.
Pia aliiomba mahakama kutoa ahirisho la mwisho kwa sababu kesi ni ya muda mrefu. Kutokana na hali hiyo, Hakimu Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 26, mwaka huu kwa ajili ya kusikilizwa.
Masogange
ataanza kujitetea baada ya mahakama kumkuta na kesi ya kujibu baada ya kusikiliza
mashahidi watatu wa upande wa mashitaka.
Masogange
anadaiwa kuwa kati ya Februari 7 na 14, mwaka jana katika maeneo yasiyojulikana
ndani ya jiji la Dar es Salaam alitumia dawa za kulevya aina ya Heroin (Diacety
Imophine).
Pia
anadaiwa kuwa kati ya Februari 7 na 14, 2017 alitumia dawa za kulevya aina ya
Oxazepam.
No comments:
Post a Comment