Serikali yaagiza kupitiwa upya mkataba Polisi na Ashoki Leyland...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

SERIKALI imeagiza kupitiwa upya mkataba wa ununuzi wa magari ya jeshi la polisi nchini na Kampuni ya kutengeneza magari ya Ashoki Leyland ya nchini India
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
 Hamad Masaun akifafanuliwa jambo na Kaimu Meneja wa Bandari, Fredi Liundi jijini Dar es Salaam.

Pia imeagiza uundwajia tume ya wataalam kuchunguza ubora wa magari 53 maarufu ya Magufuli yaliyotolewa bandarini na kupelekwa chuo cha polisi Kurasini baada ya kubainika magari matano kuwa mabovu.

Maagizo hayo yametolewa leo jijini Dar es Salaam na Naibu waziri wa wizara hiyo, Hamad Masaun alipofanya ziara ya kuona utekelezaji wa maagizo ya Rais John Magufuli ya kuyaondoa magari hayo bandarini kwenda mahali husika kwa ajili ya matumizi iliyokusudiwa.

“Magari mengi niliyoyaona hapa ni maroli, lakini tunahitaji magari madogo pia, nitoe maalekezo kwa katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi, kuundwa kamati ya wataalamu kuangalia mkataba wa utaratibu wa jinsi ya uingizaji magari haya,” amesema Masaun.

Amesema kamati hiyo itapata nafasi ya kukaa pamoja na wasambazaji hao ili kuupitia makataba kwa ajili ya maslahi ya pande zote lakini pia kuona kama unakidhi mahitaji ya sasa.

Akizungumzia hatua ya kuagiza kuundwa kwa tume ya wataalamu wa kuchunguza ubora wa magari hayo 53, amesema agizo hilo limekuja kutokana na mashaka juu ya magari hayo baada ya kupata maelezo kutoka kwa kampuni ya Ashoki Leyland  juu ya ubovu wa magari hayo matano kutokana na uchunguzi wao.

Katika hatua nyingine ametaka magari mengine 119 ambayo bado yapo bandarini yaliyoingia baada ya agizo la rais Magufuli, kufanyiwa utaratibu wa haraka wa kuyaondoa ili yakatumike.


Mwishoni mwa mwaka jana rais Magufuli alifanya ukaguzi wa ghafla Bandari ya Dar es Salaam na kukuta magari 53 aina ya Suzuki ambayo ni maalumu kwa kubebea wagonjwa na maroli zaidi ya 50 ya jeshi la polisi yaliyoagizwa tangu mwaka 2015 lakini yalikuwa bado hayajatolewa bandarini.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search