Waziri mkuu aagiza mhandisi achukuliwe hatua ....soma habari kamili na matukio360....#share
Na
Mwandishi Wetu, Mara
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Ofisi ya waziri mkuu, ametoa uamuzi huo
jana jioni wakati aliposimamishwa na umati wa wananchi kwenye mji Mdogo wa
Shitari alipokuwa njiani kuelekea kwenye kijiji cha Bubombi wilayani Rorya.
“Hatuwezi
kuwa na mtumishi wa aina hii ambaye kila eneo tunakutana na changamoto za maji
huku kukiwa hakuna hatua zinazochukuliwa licha ya Serikali kutoa fedha, hivyo
namuagiza Katibu Tawala wa Mkoa alete mhandisi mwingine wa maji.”
Pia
Waziri Mkuu amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Profesa
Kitila Mkumbo kwenda wilayani Rorya na kukagua mradi wa maji katika mji Mdogo
wa Shirati na kuona namna ya kuutekeleza.
Amesema
kwa sasa Serikali inatekeleza Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua
mama ndoo. Kampeni hiyo inalenga kuwaondolea wananchi tatizo la upatikanaji
wa huduma ya maji safi na salama, hivyo itawachukulia hatua wote
watakaokwamisha miradi ya maji.
Awali, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima alimueleza Waziri Mkuu kwamba changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika mkoa huo inatokana na watendaji wa idara hiyo kutokuwa na uwezo wa kutosha kiutendaji.
Wilaya ya Rorya inatekeleza miradi 11 ya maji ya bomba kupitia Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RWSSP) katika vijiji vya Kinesi, Randa, Utegi, Mika,Kirogo, Nyihara, Kisumwa,Nyamkonge, Nyambori, Gabimori na Marasibora.
No comments:
Post a Comment