Staa Jacqueline Wolper’ ‘Vyamshuka’ baada ya madai ya kunuka mwili’.. asema ‘Mbona Mabwana Wananipapatikia..!’
Staa wa filamu ‘grade one,Jacqueline Wolper’ ametokwa povu
si la nchi hii baada ya kubanwa kuhusiana na madai ya kunuka mwili na kusema
hajawahi kunuka maishani mwake na kwamba ingekuwa hivyo asingepapatikiwa na
wanaume. Hivi karibuni gazeti la mambo ya udaku la global Ze Ijumaa,
lilimfungia kazi msanii huyo nyumbani kwake na katika moja ya maswali
aliyobanwa lilikuwa juu ya ishu iliyosambaa kuwa eti anatoa harufu mbaya sehemu
za mwili wake.
Katika kuonesha kumaindi ile mbaya kuhusu madaia hayo,
mrembo huyo ambaye kiukweli yuko bomba kwa muonekano alifunguka: “Aliyekuambia
nanuka nani? Mimi sinuki wala sijawahi kunuka maishani mwangu, kuthibitisha
hilo kwanza nisingekuwa napapatikiwa na wanaume kila kukicha sambamba na
kuhongwa vitu kibao huku wengine nikiwaacha wakinililia.
Hao wanaosema na kusambaza hayo ni njia tu ya kujipatia
followers kwenye mitandao yao kupitia nyota yangu”… Wolper hakuishia hapo aliendelea kumwaga povu
kuwa, tangu afungue duka lake nguo ambalo amewekeza zaidi ya shilingi milioni
60, watu wengi wamekuwa wakichukizwa na maendeleo hayo. “Wana chuki tu na mimi,
tangu nimefungua duka wananichokonoa, wanalishadadia hili jambo kisa tu
nimepata mafanikio ya kufungua duka,” alipigilia msumari.
credit: QON na global
No comments:
Post a Comment