UPDATES: Jua hapa safari nzima ya Tundu Lissu kuelekea Nairobi kwa matibabu ilivyokuwa...#share

Habari, Mh Tundu Lisu aliwasili usiku majira ya saa Saba hapa Nairobi Jomo Kenyatta International Airport na alipokelewa na team ya Madaktari wa Nairobi hospital pale airport na matibabu yalianza Mara moja kuanzia ndani ya Ambulance hadi hospital.

Aidha alipofika Nairobi hospital alifanyiwa vipimo vyote na baadae saa nne asubuhi aliingizwa theatre. Tangu Jana alipofika alifanyiwa stabilization ili aweze kukabiliana na surgery na zoezi hilo lilifanikiwa vizuri na madaktari wametueleza kuwa hakuna hali yoyote ya hatari na matibabu yake yanaendelea kwa mafanikio.

Hadi sasa majira ya saa 9 alasiri bado hajatoka theatre na madaktari wametueleza kuwa wanaendelea vizuri. Nitawajuza atakapo toka theatre.

Chakushangaza hadi sasa tangu tuwasili hatujapata ushirikiano wowote wa ubalozi wa Tanzania hapa Nairobi, Si kwa balozi au maafisa wowote wale wa ubalozi. Mh Freeman Mbowe amezungumza na vyombo mbali mbali vya habari pia taarifa yake itatoka punde.

Hemed Ali 
Mkuu wa Idara ya Uenezi CHADEMA.

Nairobi hospital.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search