Nape aitaka serikali kukomesha vitendo vya kupigana risasi...Adai wahalifu wamo ndani ya serikali...#share

ALIYEKUWA Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ameitaka serikali kukomesha  vitendo vya uhalifu vya kupiga watu lisasu na kuwaonyesha silaha za moto  ilikujitenga nao.

Kauli hiyo imekuja siku moja baada Mwanasheria Mkuu wa Chama Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Na Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kupigwa lisasi na watu wasiojulikana.

Akizungumza leo mjini Dodoma Nape amedai kuwa wahalifu hao huenda wako ndani ya serikali na kusema kwamba jambo hilo siyo la kulifumbia macho kwani hakuna mtu aliyeko salama.

“Wito kwa serikali ni lazima jambo hilo walikomeshe ili serikali ijitenge na watu hao na inawezekana wamo ndani ya serikali humo humo,”

“Lakini siamini kama wanatumwa kufanya haya sasa kama watu wanafanya haya na wamo ndani na serikali isipojitenga nao mana yake itakuwa sehemu yao na ikiwa sehemu yao itakuwa jambo baya sana,” amesema Nape.

Akizungumzia kupigwa risasi kwa Lissu, amesema tukio hilo ni moja tukio la  hovyo kutokea nchini na alikumbusha kwamba alipottolewa yeye silaha hadharani alisema kama mambo hayo hayatakomeshwa, ipo siku mtu  mwingine akapigwa risasi.

Nape amesema  tukio hilo linashtua na linaumiza huku akibainisha, Lissu ni mmoja wa watu waliolalamika kuwa amekuwa akifuatiliwa na watu na kutaja  namba na ragi ya gari inayomfuatilia pamoja na idadi ya watu lakini cha kusikitisha ni kwamba hakuona hatua zilizochukuliwa na kueleza kuwa vyombo husika walizpuuza taarifa hizo.

Ameongeza kuwa  kwa mtindo huo huo jana alikuwa akifuatiliwa nyuma na gari na waliokuwemo wakampiga risasi hivyo akaeleza kwamba jambo hilo siyo dogo.

Hivyo uamuzi wa bunge wa kulipeleka suala hilo kwenye kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama na kueleza kuwa ni Imani yake kwamba baada ya hapo hatua zitachukuliwa.

Amesema kuwa wametoa hatua zichukuliwe ilikukomesha jambo hilo kwani lisipo komeshwa litaendelea kujenga chuki kati ya watanzania na serikali yao na kati ya watanzania na chama kilichounda serikali.

Aidha amesema tukio hilo linapeleka sura mbaya ya Tanzania duniani na watu kuweka dhana kwamba wanaweza kuwa nchini na kupugwa risasi mchana kweupe na waliokupiga wakaitwa wasio julikana.

Na Abraham Ntambara



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search