Dk.Tizeba afukuza maofisa watatu...Soma habari kamili na Matukio360..#share

WAZIRI wa Kilimo Dk. Charles Tizeba amemuagiza Katibu m Mkuu wa wizara hiyo Methew Mtigumwe  kuwafukuza kazi Maofisa watatu wa Idara ya Maendeleo ya Mazao katika sehemu ya pembejeo ambao wamebainika kuhusika na ukiukwaji wa sheria, Kanuni na taratibu zilizowekwa.
Waziri wa kilimo Dk. Charles Tizeba (katikati) akisisitiza jambo Wakati wa Mkutano na waandishi wa habari Mjini Geita, Mwingine ni Naibu Waziri wa wizara hiyo Dk. Mary Mwanjelwa (Kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya kilimo Mhandisi Methew Mtigumwe.

Agizo hilo limetolewa leo na Waziri Tizeba akizungumza na waandishi wa habari mjini Geita, amesema maofisa hao walikosa umakini  katika usimamizi wa sheria ya ununuzi wa Umma.

“….ikiwemo kusababisha kuchapishwa kwa vocha za pembejeo zenye thamani ya Tshs 78,054,970,000 ambazo ni zaidi ya bajeti halisi iliyotengwa kwa ajili ya ruzuku ya pembejeo kwa kiasi cha Tshs 42,587,419,200,” amesema Tizeba.
Maafisa waliofukuzwa kazi ni  Shenal S. Nyoni aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi wa kitengo cha pembejeo, Michael G. Mayabu aliyekuwa Afisa kilimo Daraja la I na Bw Michael G. Mayabu na Franks F. Kamhabwa.

Aidha Tizeba ametoa agizo hilo baada ya kupitia taarifa ya waraka wa mkakati wa utekelezaji na usimamizi wa utoaji wa Ruzuku za pembejeo za kilimo kwa wakulima kwa kutumia vocha wa mwaka 2015/2016 ambapo pamoja na mambo mengine uliainisha utaratibu wa usimamizi wa zoezi la utopaji wa ruzuku ambao ulilenga kuleta ufanisi katika utekelezaji wake.

Katika hatua nyingine Tizeba waziri huyo amemuagiza katibu Mkuu Mtigumwe kuwasimamisha kazi watumishi wengine watatu ambao ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mazao  Twahir S. Nzallawahe, Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi Burhan A. Shaban na Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha pembejeo  Canuth Komba.

Hatua hiyo imekuja kutokana na uzembe ambao ungeweza kusababisha upotevu wa zaidi ya sh. 29,977,114,700 kwa mwaka wa  fedha wa 2015/2016 ambapo serikali ilitenga sh. 35,467,550,800 kwa ajili ya pembejeo za kilimo na mara baada ya zoezi la utoaji ruzuku ilibainika kuwa deni lililowasilishwa serikalini na mawakala ilikuwa ni kiasi cha sh. 65,444,665,500.


Sambamba na hayo Tizeba ameviomba vyombo vya dola kuchunguza zaidi na kuchukua hatua stahiki za kisheria dhidi ya watumishi na watu wote waliohusika katika ngazi za halmashauri na mawakala wote waliofanya udanganyifu kwa lengo la kuisababishia serikali hasara.

Waziri Tizeba (katikati) akisisitiza jambo Wakati wa Mkutano na waandishi wa habari Mjini Geita, Mwingine ni Naibu Waziri Mhe Dk. Mwanjelwa (Kushoto) na Katibu Mkuu Wizara Methew Mtigumwe.
Waziri Tizeba akitafakari jambo mara baada ya kuzungumza na vyombo vya habari Mjini Geita

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search