Mkuchika: Kuna rushwa kubwa Sekretarieti ya Ajira...soma habari kamili na Matukio360..#share


Na Salha Mohamed
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimanti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema Sekretarieti ya ajira inachangamoto kubwa ya kukabiliana  na vitendo vya rushwa.
 Waziri George Mkuchika (katikati) akisisitiza jambo 
 wakati akizungumza na watumishi wa Sekretarieti ya Ajira jijini Dar es Salaam.

Amesema hayo leo jijini Dar es Salaam katika ziara yake ya kuangalia utekelezaji wa majukumu ya Sekretarieti ya Ajira.
Mkuchika amesema wizara yake  ndiyo inayofuata sheria hivyo watumishi wake wanapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu na kuwa ataraji kusikia malalamiko kutoka kwa wananchi.
"Hakuna mahala penye ushawishi na kupewa rushwa kama hapa Sekretarieti ya Ajira, muwe makini na maadili kwa kutenda haki kwa wenye sifa kupata kazi, usiombe faili liletwe kama kunamtumishi kapokea rushwa, mjiepushe na rushwa na mtende haki,"amesema.
Pia amesema Serikali itarekebisha sheria za uajiri kwa watumishi wote nchini kupitia Sekretarieti ya ajira.
Hatua hiyo inatokana  na sheria iliyofanyiwa marekebisho ya sheria ya Utumishi wa Umma Na 8 ya mwaka 2012 yaliyofanywa kupitia sheria Na 2 ya mwaka 2013 kuwa na mapungufu.
Mkuchika amesema sheria hiyo ya uajiri inamapungufu katika kuajiri baadhi ya watumishi katika kada mbalimbali kwani wapo wanaoajiri moja kwa moja bila kupitia katika  sekretarienti hiyo.
"Kuna mapungufu ya Sheria, naahidi katika kipindi changu cha uongozi...tutayaangalia Bungeni lakini kadri tunavyoendelea zinajitokeza changamoto mbalimbali."amesema.
Kwa upande wake Katibu Sekretarieti ya Ajira Xavier Daudi amesema wamepunguza watumishi wa vyeti vya kughushi katika mchakato wa ajira serikalini kutokana na uhakiki wanaofanya .
"Haina budi kuwezeshwa katika rasilimali fedha kwa kupitia bajeti inayokidhi mahitaji ili kuongeza weledi na kutumia mbinu na mifumo mipya na ya kisasa kwenye mifumo yake ili kupata rasilimali watu waliokidhi mahitaji ya sasa,"amesema.


Waziri George Mkuchika akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Sekretarieti ya Ajira Jijini Dar es Salaam.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search