Mhasibu wa ubalozi wa Tanzania nchini Msumbiji atuhumiwa kuchota mamilioni..Apandishwa kizimbani..Soma habari kamili na Matukio360..#share



JOYCE Moshi(56) ambaye ni Mhasibu wa Ubalozi wa Tanzania nchini  Msumbiji, amepandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akikabiliwa na mashitaka tisa ikiwamo la utakatishaji fedha wa dola za Marekani 150,000.



Miongoni mwa mashtaka mengine yanayomkabili ni kughushi, kuwasilisha nyaraka za kughushi, wizi akiwa mtumishi wa umma na utakatishaji wa fedha.



Wakili wa Serikali, Wankyo  Simon amemsomea  mashtaka yanayomkabili mshtakiwa huyo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.



Akisoma mashtaka hayo, Wakili wa Wankyo amedai  Oktoba 25, 2016 katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania zilizopo Maputo nchini Msumbiji,  mshtakiwa huyo alighushi barua ya Oktoba 25, 2016.

Akijaribu  kuonesha kuwa ofisi ya ubalozi wa Tanzania nchini Maputo Msumbiji umeilekeza Benki ya Millennium BIM ya Maputo, kuhamisha kiasi cha dola za Marekani 10,000 kutoka kwenye akaunti namba 79667362 kwenda akaunti namba 182283177 inayomilikiwa na Mushi na kwambq akaunti hizo zote  zipo kwenye benki hiyo iliyopo katika tawi la Julius Nyerere Maputo, wakati akijua si kweli.



Mshitakiwa huyo anadaiwa kuwa Februari 10, 2017 katika ofisi za Ubalozi Maputo Msumbiji, mshitakiwa huyo alighushi barua ya  Februari 10, 2017 alionyesha  kuwa ubalozi huo umeielekeza Benki ya ya Millennium BIM ya Maputo, kuhamisha dola za Marekani 10,000 kutoka akaunti namba 79667362 kwenda akaunti namba 182283177 inayomilikiwa na Moshi.



Mshitakiwa huyo anadaiwa kuwa  Aprili 12, 2017 katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania  Maputo nchini Msumbiji, alighushi barua ya Aprili 12, 2017 akijaribu kuonesha kuwa ubalozi huo umeielekeza Benki  ya Millennium BIM ya Maputo, kuhamisha dola za Marekani 40,000 kutoka akaunti namba 79667362 kwenda akaunti namba 182283177.



Oktoba 25, 2016 mshitakiwa huyo  katika Benki ya Millennium BIM iliyopo tawi la Julius Nyerere   Maputo nchini Msumbiji, aliwasilisha kwenye benki hiyo nyaraka za kughushi ambayo ni barua ya Oktoba 25, 2016 akionesha kuwa Ubalozi wa Tanzania nchini Msumbiji umeelekeza benki hiyo kuamisha dola za Marekani 10,000 kutoka kwenye akaunti ya benki hiyo kwenda kwenye akaunti inayomilikiwa na mshitakiwa huyo.

Wankyo aliendelea kudai kuwa Februari 10, 2017 katika benki hiyo, Moshi alitoa nyaraka za uongo kuonesha kwamba Ubalozi umeelekeza kuamisha dola za Marekani 10,000 kwenda kwenye akaunti ya Mushi.



Ili endelea kudai wa kuwac Aprili 12, 2017 katika maeneo ya benki hiyo mshtakiwa huyo aliwasilisha barua ya Aprili 12, 2017 kuonesha kuwa ubalozi umeelekeza kuamisha dola za Marekani 40,000 kwenda kwenye akaunti ya Moshi.



Wankyo alidai mshitakiwa huyo katika tarehe tofauti kati ya Oktoba 25,2016 na Aprili 12, 2017  akiwa mtumishi  wa umma kama Mhasibu wa Ubalozi wa Tanzania nchini Msumbiji, aliiba dola za Marekani 150,000 mali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.



Inadaiwa kati ya Oktoba 25, 2016 na Aprili 12, 2017 katika ofisi za ubalozi huo, Moshi alijipatia dola za Marekani 150,000.



Wanadaiwa kuwa,  kati ya Oktoba 25, 2016 na Aprili 12, 2017 katika ofisi za Ubalozi wa Tanzania uliopo Maputo nchini Msumbiji na Benki ya Millenium BIM tawi la Julius Nyerere Maputo, alijipatia dola za Marekani 150,000 wakati akijua fedha hizo ni zao la  kughushi.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mshitakiwa huyo alikana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kwamba tarehe ijayo wataeleza  hatua zilizofikiwa.



Wakili wa utetezi, Jebra Kambore aliomba upande wa mashtaka wajitahidi kukamilisha upelelezi kwa wakati.



Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 31, 2017 kwa ajili ya kutajwa. Mshitakiwa alipelekwa Mahabusu.






















About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search