Auwawa akituhumiwa kuiba kuku ...soma habari kamili na matukio360...#share



Na Mwajuma Juma, Zanzibar
WATU wawili wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti Visiwani Zanzibar likiwamo la wizi wa kuku.

Kamanda Hassan Bashir

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa mjini Magharibi, Hassan Nassir amemtaja marehemu huyo kuwa ni Ali Simai Khamis (28) mkazi wa Kama ambaye alifariki dunia kutokana na majeraha baada kupigwa na watu wasiojuulikana.

Amesema marehemu alichomwa na kitu chenye ncha kali mguu wa kushoto na kushambuliwa sehemu mbali mbali za mwili wake kwa mawe na marungu pamoja na kufungwa kamba mikononi.

Kwa mujibu wa kamanda Nassir sababu ya shambulio hilo ni kuiba kuku na kwamba watu wawili wamekamatwa  na uchunguzi unaendelea.  Tukio hilo limetokea Januari 16, 2018 

 Mwingine aliyefariki ni Majaliwa Hussein (34) mkazi wa Chalinze
Dar es  Salaam ambaye alikutwa amekufa  Forodhani nyuma ya Hoteli
ya Tembo, alipokuwa akiogelea na wenzake.

Amesema  mwili wa marehemu ulifikishwa katika Hospitali ya Mnazi
mmoja kwa uchunguzi na kukabidhiwa ndugu zake kwa mazishi, tukio
 lilitokea Januari 19 mwaka huu majira ya saa 9:00 za Alasir.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search