Onesho chimbuko la binadamu kuonyeshwa bure DSM...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

MAKUMBUSHO ya Taifa  kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Ubalozi wa Hispania nchini imeandaa onesho la chimbuko la binadamu barani Afrika pamoja na semina. Litafanyika kesho jioni Januari 23, 2018.


Mkurugenzi Mkuu wa makumbusho ya taifa, Profesa Audax Mabulla akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Profesa Audax Mabulla alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, amesam semina na onesho hilo ni matokeo ya tafiti mbalimbali zinazofanyika bonde la Olduvai na Laetoli na hifadhi ya mamlaka ya Ngorongoro.

“Onesho hili litafunguliwa rasmi na Dk.Hamis Kigwangalla, waziri wa maliasili na utalii kesho saa 11 jioni hapa Makumbusho ya Taifa,” amesema Prof. Mabulla.

Amesema onesho limegawanyika katika sehemu nne zanazowiana. Sehemu ya kwanza litahusu ushahidi wa nyayo za binadamu zilizogunduliwa huko Laetoli mwaka 1978 na mtafiti Dk. Mary Leakey.

Sehemu ya pili itahusu hadithi ya kusisimua ya kuwa binadamu (Genus Homo) ambapo kuna masalia ya binadamu Zinjanthropus au Paranthropus na Homo habilis, zana za mawe za mwanzo (Oldwan) zilizotumika katika kujipatia chakula na ushahidi wa kale wa ulaji wa nyama katika historia ya mabadiliko ya binadamu, takribani miaka milioni 2 iliyopita.

Amesema sehemu ya tatu itahusu maisha ya jamii ya Homo erectus. Jamii hii inafanana zaidi na binadamu wawa sasa kuliko jamii zilizotangulia.

Na sehemu ya nne amesema itaonesha kipindi cha mwanzo cha binadamu wa sasa (Homo sapiens) walioanza kutokea Afrika miaka laki 2 iliyopita.


Profesa Mabulla amewaomba wananchi na wadau mbali mbali kujitokeza katika onesho na semina  na kwamba itakuwa bure.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search