Tetesi za soka Ulaya leo Alhamisi.... soma habari kamili na matukio360...#share

Na mashirika ya kimataifa
WINGA wa Chelsea Mbrazil, Willian (29) anaweza kuiacha timu hiyo katikati ya mwaka na huenda akujiunga na timu ya AC Milan au Manchester United (Star)

Willian
Manchester United wameongeza muda ya mikataba ya mchezaji Ashley Young, 32, na Daley Blind, 27, na ule wa mlinda mlango Sam Johnstone, 24
Mashetani hao wekundu wana mipango wa kumuacha  kiungo Marouane Fellaini, 30, na Michael Carrick, 36, na mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic ambao watakuwa huru kuondoka na kwa usajili huru majira ya joto.
Manchester United wataachana na mpango wa kuupanua uwanja wa Old Trafford mwaka huu na kujikita zaidi katika kumuunga mkono Jose Mourinho katika kutafuta wachezaji.(Mail)
Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake.
Hata hivyo Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal
Kibarua chake kimewekwa matatani wakati alipokataa kuthibitisha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror)
Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)
West Ham iko tayari kumsiani mlinzi wa Ireland Kaskazini Jonny Evans, 30, kwa paundi milioni tatu kutoka kwa West Brom ikifika mwisho wa msimu. (Birmingham Mail)
Kiungo wa Arsenal na timu ya England, Jack Wilshere, 26 anasema atatoka kwenye klabu hiyo kati kati ya mwaka huu, wasipo mpatia mkataba bora zaidi. (Sun)

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search