LHRC: Uchaguzi Kinondoni, Siha ulivunja sheria, haki za binadamu...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
KITUO cha Sheria na
Haki za Binadamu (LHRC) kimedai uchaguzi mdogo wa marudio ya ubunge katika jimbo la Siha na Kinondoni uligubikwa na ukiukwaji wa haki za binadamu,
sheria na taratibu zinazoratibu chaguzi.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga akionesha waandishi wa habari jijini Dar es Salaam nakala ya ripoti ya uchaguzi wa marudio ya ubunge wa Kinondoni na Siha uliofanyika Februari 17, 2018.
Hayo yamesemwa leo
jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga alipokuwa
akitoa ripoti ya uchaguzi huo uliofanyika Februari 17, 2018 mbele ya waandishi
wa habari.
“Katika kutimiza jukumu
hilo la kidemokrasia, LHRC kimefanya uangalizi tangu zilipoanza kampeni mnamo Januari
25, 2018 na wakati wa uchaguzi ambapo katika chaguzi hizo ndogo chama cha
Mapinduzi kilishinda. Hata hivyo LHRC kimebaini masuala kadhaa ya ukiukwaji wa
haki za binadamu na ukiukwaji wa sheria na taratibu zinazoratibu chaguzi kama
zilivyoainishwa,” amesema Henga.
Amesema wakati wa
kampeni kulishuhudiwa kutumika kwa watoto suala ambalo ni kinyume na kifungu
namba 12 cha sheria ya mtoto, 2019 kinachokataza kuwaajiri watoto katika
shughuli yoyote ile ambayo ni hatarishi kwa maslahi mapana ya mtoto, kiafya,
kielemu kiakili, kimwili pamoja na maendeleo ya kimaadili.
“LHRC kimeshuhudia
video ya mtoto mdogo aliyekuwa jukwaani akitumika katika mkutano wa kampeni wa
Chama cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika Makumbusho katika jimbo la kinondoni
Februali 2, 2018. Huu ni ukiukwaji wa haki za binadamu hususani haki za watoto,”
amesema.
Henga ameongeza kuwa
kulikuwa na matumizi ya rasilimali za umma kwa maslahi ya vyama ambapo amesema
kuwa viongozi wa serikali walitumia magari ya umma katika mikutano ya kisiasa
kinyume na sheria ya vyama vya siasa na sheria ya uchaguzi haswa sheria ya
gharama za uchaguzi ya mwaka 2010.
Amesema pia kulikuwa na
matumizi ya nguvu yaliyopelekea watu kujeruhiwa na kuuawa ambapo ameeleza kuwa
matumizi hayo ya nguvu yalitumika kipindi cha kampeni na kupelekea raia
kuumizwa na hatimaye vifo. Ametoa mfano kuwa ni kuuawa kwa mwanafunzi wa NIT
Akwilina Akwilini aliyeuawa na polisi wakisambaratisha waandamanaji wa Chadema na kuwashikilia wafuasi 40 wa chama hicho.
Kipindi
cha Uchaguzi
Amesema wakati wa
uchaguzi walibani dosari kadhaa zikiwemo, mwitikio mdogo wa wapiga kura, unyanyasaji wa
mawakala wa vyama vya siasa, uwezo mdogo wa wasimamizi wa uchaguzi, mazingira
yasiyo rafiki kwa wapiga kura na watu wenye ulemavu.
Nyingine ni uwepo wa
mabango ya wagombea katika vituo vya kupigia kura, kutokuwepo kwa usiri katika
eneo lakupigia kura, uwepo wa polisi wengi vituoni, kupotea kwa shahada na
vituo kutofunguliwa kwa wakati.
Mapendekezo
Kutokana na changamoto
hizo LHRC kimetoa mapendekezo kadhaa ikiwa ni pamoja na Tume ya Uchaguzi kutakiwa
kuratibu chaguzi mbalimbali kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni zilizopo
bila kufungamana na itikadi zozote za vyama vya siasa.
Vyama vya siasa
hususani chama tawala kuacha kutumia rasilimali za umma hasa katika kipindi cha
kampeni na vyama vya siasa kujikita katika kuhubiri Ilani za vyama vyao na
kuacha kutumia kejeli, matusi na vijembe katika kampeni.




No comments:
Post a Comment