Kuna taarifa ya ajali mbaya ya basi aina ya Coaster likiwa limebeba wanafunzi maeneo ya Karatu



Tumepata taarifa muda huu kuna ajali mbaya imetokea maeneo ya karatu basi la shule limeanguka kabla ya kuingia karatu mjini na kuua watoto wengi ambao idadi yake bado haijafahamika. Wanafunzi hao wanaokadiriwa kuwa wa darasa la 7 inasemekana ni wa shule inayoitwa Lucky Vicent ya Arusha ambao walikua wanaenda karatu kufanya mitihani ya mashindano na shule za karatu. Kwa mujibu wa shuhuda basi hilo lilikua limebeba watoto zaidi ya 40 na wengi wao (zaidi ya nusu) inasemekana wamepoteza maisha akiwemo dereva na walimu… tuendelee kupashana kwa karibu na kuwaombea majeruhi
Source: JF


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search