Baada ya Mbunge Nkamia 'kutibua hali ya hewa' kwa hoja ya u-Rais kuwa Miaka 7... Mbunge Henche Chadema kamjibu na hoja ya ukomo wa u-Rais wa miaka 4... Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360...#share

SIKU chache baada ya Mbunge wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi  (CCM) kutangaza dhamira yake ya kuwasilisha hoja binafsi Bungeni ya kutaka kuongezwa kwa muda wa Rais kuwa madarakati kutoa miaka mitano ya hivi sasa hadi saba.

Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche naye ameonyesha dhamira yake ya kupeleka hoja binafsi bungeni ya kupunguza muda wa kuwa madarakani kwa Wabunge na Madiwani kutoka miaka mitano hadi ya hivi sasa hadi minne.

"Nakusudia kuwasilisha bungeni hoja binafsi kupunguza mda wa kukaa madarakani kwa rais, wabunge na madiwani kutoka miaka 5 mpaka 4 tuwe kama Marekani ili kutoa nafasi kwa wananchi kuwa na maamuzi zaidi kuhusu uendeshaji wa nchi yao," ameandika Heche kupitia ukurasa wake wa faceebook.




Hivi karibuni Nkamia alithibitisha dhamira yake ya kutaka kupeleka hoja binafsi ya kuhusu ukomo wa muda wa Rais Kuwa Madarakani uongezwe kutoka miaka mitano ya hivi sasa hadi miaka 7 kama ilivyo kwa nchi ya Rwanda, jambo ambalo lilizua mjadala mkubwa nchini huku walowengi wakipinga hoja hiyo kwani inataka kusababisha uvunjifu mkubwa wakatiba.


Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search