Exclusive:(+Audio) Maajabu ya Msukule - Msanii Popo Michael wa Geita afariki na kuzikwa, kisha apatikana Nyankumbu akiwa hai.. haya hapa ndio mahojiano yake na mwandishi maalum wa Matukio360.. #share

MSANII wa nyimbo za asili mkoani Geita Daniel Matunge almaarufu kama Popo Michael anaishi katika hali ya mateso kutokana na kile alichoeleza kusafirishwa kwa njia ya aanga kimazingara kutoka Kahama Mkoani Shinyanga hadi Nyankumbu mkoani Geita huku wazazi wake wakiwa na taarifa za kuwa amefariki dunia.



Akizungumza kwa taabu nyumbani kwa baba yake mdogo Paschal Matunge katka kijiji cha Mwenegeza kata ya Nyakagomba tarafa ya Butundwe , Msanii huyo alijikuta katika hali isiyoeeweka akiwa mjini Kahama Mkoani Shinyanga baada ya kusalimiana na watu wawili mke na mme ambao hakuwatambua.

Ameelza kuanzia hapo alijikuta akiwa angani katika chombo kisichofahamika na kutupwa chini katika ardhi ya Nyankumbu mkoani Geita.

Amesema tukio hilo lilimkuta siku ya Ijumaa, na akaokotwa siku ya jumamosi majira ya asubuhi akiwa na pamba mdomoni, puani na masikioni mithili ya maiti.

Baba mzazi wa Msanii huyo Michael Matunge amesema kabla ya kuokotwa kwa mtoto wake, alipokea simu na ujumbe wa maadishi sms ukimtaarifu kuwa kijana wake amefariki na kwamba mwili wa marehemu upo katika Hospitali ya wilaya Kahama ambapo ndugu zake walifuatilia nakubaini kuwa ni uwongo.

Baba mzazi wa Popo Michael


Msanii huyo anayefahamika kwa jina la Popo Michael ana wake wawili.

Hamisa Sadiq  ni mke mkubwa, anahusisha tukio hilo na imani za kishirikina kwa kuwa siku ya Ijumaa usiku alimuona mme wake akiwa ndani amekaa kwenye kiti, na alipotoka nje kwaajili ya haja ndogo hakumuta hadi asubuhi zilipopatikana taarifa kuwa amefariki na mwili kuokotwa Nyankubu ukiwa na pamba masikioni, puani na mdomoni.

Hata hivyo, Daniel Michael Matunge  almaarufu kama Popo Michael anaeleza kuwa kutokana na kudondoshwa chini akitoka angani kwenye chombo cha usafiri ambao hakukitaja anaumia sehemu mbali mbali za mwili kama vile,Mgongo,kiuno,miguu,kichwa na shingo.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search