Profesa Jay Atia Neno Saka la Zari, Diamond na Hamisa Mabetto...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360...#share

MBUNGE wa Mikumi mkoani Morogoro na Mwanamuziki nguli wa  wa HipHop nchini Joseph Haule a.k.a Professor Jay amemuunga mkono msanii wa muziki wa kizazi kipya Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kwa kitendo chake cha kuweka wazi kuwa mtoto wa Mwanamitindo  Hamisa Mobetto ni wake.
Profesa Kupitia mitandao yake ya kijamii ya Instagram na Facebook ameandika maneno haya “Ukweli humuweka Mtu huru KWELIKWELI.. Big up mdogo wangu @diamondplatnumz  Umekuwa Mfano bora sana.”

Itakumbukwa jana Diamond akiweka wazi suala hilo  wakati akiendelea na mahojiano katika kituo cha Clouds FM, Zari aliandika katika mtandao huo akisema, “Hahahaha unajidanganya, unasema uongo kuhusu mimi kujua kuhusu michepuko yako, malizana na balaa ulilolianzisha. Mimi kunyamaza haimaanishi ni mpumbavu. Kuwa makini na maneno yako.”

Aliendelea kuandika: “Inawezekana mimi ni mama wa watoto wako ndio maana nimeamua kunyamaza kimya. Labda ugoogle kuhusu ‘defamation of character law suit’, usinijaribu.”


Na Mwandishi wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search