LHRC Yavitaka Vyombo Vya Ulinzi na Usalama Kuchukua Hatua Dhidi ya Wahalifu...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360...#share

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeviomba vyombo vya ulinzi na usalama nchini  kuwachukulia hatua kali watu wote wanaoshiriki katika vitendo vya uhalifu.

Related image

Ombi hilo limetolewa jijini dar es salaam na mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu dkt hellen kijo bisimba wakati akitoa tamko la maadhimsho ya siku ya amani duniani.

Dkt. Kijo-Bisimba amesema endapo vitendo vya uvunjifu wa amani vinavyoendelea kufanywa na baadhi ya watu nchini vitafumbiwa macho vinaweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Aidha bi kijo amewataka wananchi kutambua kwamba wao ndio walinzi wa kwanza wa amani nchini hivyo wanapaswa kufuata sheria na kuepuka vitendo vya kujichukulia sheria mkononi.
Kila ifikapo septemba 21 dunia huadhimisha siku ya amani duniani ambapo kwa mara ya kwanza iliadhimishwa mwaka 1981 baada ya kuidhinishwa na mkutano mkuu wa umoja wa mataifa ikiwa na lengo la kuimarisha wazo la amani ndani ya baraza la umoja wa mataifa.


Kauli mbiu ya siku amani duniani kwa mwaka 2017 ni “pamoja kwa ajili ya amani, nidhamu, usalam na heshima kwa wote”




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search