Real Madrid yaondolewa kuwania taji La Liga...soma habari kamili na matukio360..#share
Na mashirika ya kimataifa
TIMU ya Real Madrid imepoteza matumaini ya kuwania taji
la ubingwa wa La Liga baada ya leo kukubali kichapo cha bao 3-0 kutoka kwa Barcelona.
Sasa Barcelona inaongoza ligi mbele ya Real Madrid iliyonafasi ya nne kwa tofauti ya pointi 14.
Lionel Messi akifanya vitu vyake mbele ya wachezaji wa Real Madrid
Barcelona iliyokuwa ugenini ilionyesha mchezo mzuri na shambulio la kipindi
cha pili cha mchezaji Luis Suarez na
penalti ya Lionel Messi baada ya Dani Carvajal kupewa kadi nyekundu kwa kunawa
mpira, bao lililosaidia Barcelona kupanda juu ya jedwali kwa alama 14 dhidi ya
Real.
Karim Benzema alipiga mwamba wa goli na kukosa nafasi
mbili za wazi katika kipindi cha kwanza , lakini timu hiyo ya nyumbani ilibaki
bila jibu katika mechi hiyo ya El Clasico.
Los Blancos ilianza huku
Gareth Bale akiwa benchi, na ijapokuwa alimlazimu kipa Marc-Andre ter Stegen
kuokoa mipira baada ya kuingizwa kufuatia kutolewa kwa Carvajal, mshambuliaji
huyo wa Wales alishindwa kuokoa timu yake.
Badala yake mchezaji wa
ziada Aleix Vidal aliongeza chumvi katika kidonda katika dakika za lala salama
kwa kupata bao la tatu.
Ni mara ya kwanza kwa Barcelona
kushinda mechi tatu za ugenini
mfululizo katika uwanja wa Bernabeu, na matokeo hayo yanakiwacha kikosi cha
Zinedine Zidane katika nafasi ya nne.




No comments:
Post a Comment