Tshishimbi mchezaji bora Februari....soma habari kamili na matukio360...#share


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

KIUNGO wa Yanga SC, Papy Kabamba Tshitshimbi amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa mwezi Februari, mwaka huu.
Papy Kabamba Tshitshimbi 

Mchazaji huyo raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ametwaa tuzo hiyo akiwashinda mshambuliaji Mganda wa Simba, Emmanuel Okwi na kiungo mwenzake wa Yanga, Pius Buswita. 

Katika mwezi Februari, Okwi aliongoza kwa kufunga mabao, akifunga mara nne akifuatiwa na Tshishimbi matatu na Buswita mawili.

Lakini Tshishimbi alikuwa na pasi ya bao(assist) pia kwenye mwezi huo na bahati nzuri kwake hakuonyeshwa kadi yoyote, wakati Okwi alionyeshwa kadi ya njano.

Kingine kilichombeba Tshishimbi kumbwaga Okwi ni kuiwezesha Yanga SC kukusanya pointi 12 Februari, wakati Simba ilivuna pointi 10 tu.

Kwa ushindi huo, Tshishimbi atazawadiwa fedha taslimu Sh. Milioni 1 kutoka kwa wadhamini wa Ligi hiyo, Kampuni ya Vodacom Tanzania pamoja na kisimbuzi (decoder) kutoka kwa wadhamini wa matangazo wa Ligi hiyo, Azam TV na ngao ya kumbukumbu ya ushindi wake.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search