BIMA YA MAZAO: MKOMBOZI MPYA WA WAKULIMA TANZNIA.

PATA KUFAHAMU UWEPO WA FAIDA KUBWA KWA WAKULIMA ITOKANAYO NA BIMA YA MAZAO YA BIMA YA MAZAO KWA WAKULIMA!!

Mtandao wa Vikundi Vya Wakulima Tanzania (Mviwata) , umewataka wakulima nchini kujiunga na bima ya mazao ili kujikinga na majanga mbalimbali ikikwemo mabadiliko ya tabia nchi ambayo namechangia ukame na mafuriko hapa nchini.

Mwenyekiti wa Mviwata ngazi ya Taifa, Veronica Sophu, alisema hayo wakati wa kufunga Mradi wa majaribio unaoshughulikia  changamaoto za wakulima ujulikananao kama FARMAF.
Mradi huyo wa FARMAF umefanya kazi katika mikoa mitatu kupitia vikundi vya wakulima.
“Bima ya  mazao, itamsaidia mkulima pale atakapo pata majanga mbalimbali yakiwemo yanayotokana na mabadiliko ya tabia nchi, mafuriko na ukame, hivyo nawashauri wakulima wajiunge na bima hii kwa sababu ni mkombozi pale kunapotokea majanga” alisema
Sophu alisema hapa nchini, mradi huo  ulioanza mwaka 2014 na kukamilika Desemba mwaka 2016 na ulifadhiliwa na Jumuia ya Ulaya na ulijikita katika maeneo matatu ambayo ni Stakabadhi ghalani, bima ya mazao na mfumo wa masoko unaotumika.

“Mradi huu, hapa nchini umetekelezwa katika wilaya tatu za mikoa mitatu ambazo ni Mtwara(Masasi ), Manyara(Kiteto) na Dodoma kupitia wilaya ya Kongwa na umekuwa na mafanikio makubwa kwa wakulim”alisema Sophu.
Kwa upande wake,  Apolo Chamwela  ambaye ni  mkulima wa Mahindi kutoka kijiji cha Magumu wilaya ya Kiteto alisema kupitia bima ya mazao ambayo wameikata katika msimu wa mwaka huu, wanaamini itawasaidia kwa sababu kiasi cha fedha wanachowekeza katika mashamba hakitapotea kutokana na majanga mbalimbali yanayotokea ikiwemo ukame na mafuriko.

“ Kupitia mradi huu wa bima ya mazao,wakulima zaidi ya 44 kutoka kijiji  cha Magumu kilichopo wilaya ya Kiteto ambapo mradi huu wa majaribio unatekelezwa , tayari wamejiunga na bima”alisema Chamwela.
“Bima hii ni asilimia nane ya gharama ya mkulima anazotumia katika kilimo na kwamba mtu anakata bima kulingana na gharama za uzalishaji kwa wale wakulima ambao wanalima kisasa, heka moja ina gharimu Sh 307000, kwa maana hiyo mkulima atakata bima ya Sh 24560 kulinda gharama ya hiyo heka moja”aliongeza Chamwela
Naye,  Mratibu wa Mradi huo wa Farmaf kutoka Chuo Kikuu cha Greenwich nchini Uingereza, Dk Gideon Onumah alisema katika bara la Afrika mradi huo umetekekezwa katika nchi tatu ambazo ni Tanzania, Zambia na Bukinafaso.
”Nchi ya Zambia, wakulima wake wao walikata bima kwenye mikopo ya kilimo inayoendana na pembejeo lakini kwa wakulima wa Tanzania wao wamekatia bima mazao ambayo tayari wamezalisha na faida ya kukatia bima mazao ni kuwa na usalama wa mazao yao mpaka pale utakapoenda sokoni kuuza na pia kama mkulima angepata janga angefidiwa kupitia bima aliyokatwa”alisema Dk Onumah.


Makala hii imeandikwa na Mwandishi maalum!

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search