NCHI JIRANI! HOTELI YA KIFAHARI YACHOMWA MOTO


Hoteli ya kifahari yachomwa moto KenyaHaki miliki ya pichaMUKUTAN RETREAT
Image captionHoteli ya kifahari yachomwa moto Kenya
Hoteli moja ya kifahari nchini Kenya, inayomilikiwa na raia wa Italia na mwandishi wa vitabu Kuki Gallmann, imechomwa moto na watu wanaokisiwa kuwa wafugaji.
Hilo ndilo shambulizi la hivi punde katika eneo hilo linalokumbwa na ukame la Laikipia, kutoka kwa watu wanaikisiwa kuwa wafugaji ambao wanavamia mashamba ya kibinafsi wakitafuta malisho.
Hakukuwa na wageni ndani ya hoteli hiyo ya Mukutan wakati ilichomwa.
Huenda shambulizi hilo ni la kulipiza kisasi oparesheni ya polisi, ripoti zinasema.
Hoteli ya kifahari yachomwa moto KenyaHaki miliki ya pichaTHE STAR, KENYA
Image captionHoteli ya kifahari yachomwa moto Kenya
Mapema wiki hii, polisi wanaripotiwa kuwapiga risasi na kuwaua karibu ng'ombe 100 katika shamba linalomilikiwa na Bi Gallmann.
Eneo la Laikipia lenye ukubwa wa ekari 10,000, mraba ndiko wazungu humiliki mashamba makubwa.

    About Author Matukio360

    Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

    No comments:

    Post a Comment

    Leo leo Plus

    Start typing and press Enter to search