Waziri Mwijage atoa ya moyoni...Soma habari kamili na Matukio360..#share
Na Salha Mohamed
WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage
amewataka wafanyakazi nchini kutong'ang'ania kuajiriwa kwenye viwanda
wasivyokuwa na maslahi na badala yake wafungue viwanda vidogo vya
kuchakata malighafi na kuajiri watu wengi.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage.
Hayo yamebainishwa Dar es Salaam leo, wakati wa maadhimisho
ya Siku ya Haki za Binadamu Afrika yenye kauli mbiu 'Uchumi wa Viwanda na
Haki za Wafanyakazi nchini' yaliyoandaliwa na Tume ya Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora.
Amesema hapa nchini hakuna tatizo ya haki za binadamu hivyo
wananchi wanapaswa kujenga viwanda ili kukuza uchumi wa kati hadi kufikia
2025 na kuondoa vikwazo.
"Kufanya kazi kwenye kiwanda cha mtu si ndoa katoliki
kwamba haiwezi vunjika, mtoke mkafanye kwengine viwanda vingine vipo vingi
hapa nchini...uzuri wa watanzania wanafundishika, utakosa kazi kiwandani kama
ukienda kuomba kazi ukisema unataka kazi yeyote,"amesema Mwijage.
Amesema wafanyakazi wanapaswa kutojiingiza katika mikataba ya
muda mrefu kwa kufanya hivyo ni kutawafunga kutofuata fursa kwenye viwanda
vingine vyenye maslahi zaidi.
Mwijage amewataka wafanyakazi kufanya kazi kwa weledi na kuwa
na ujuzi zaidi ya mmoja kwani sheria za kuwalinda zipo na wakiona zningine
waseme ili waishi vizuri.
"Kazi ni nyingi, lakini watendaji kazi hawapo kama
vitabu vitakatifu vilivyosema, ujenzi wa uchumi wa viwanda ni zaidi ya
ujenzi wa Kiwanda vijana wawe na uthubutu na nguvu ya kutoka," amesema.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti Tume ya Haki za Binadamu na
Utawala Bora, Iddi Mapuri amesema haki za wafanyakazi zinalindwa na Katiba
na Sheria za nchi, wafanyakazi wanakabiliwa na changamoto za ubaguzi,
mazingira duni ya kazi.
"Changamoto zingine ni kutozingatiwa kwa saa za kazi
kinyume na sheria, kukosekana kwa muda wa kazi wa ziada, ujira usio
stahiki, kutokuwepo kwa vyama vya wafanyakazi katika baadhi ya
ajira,kutozingatiwa ipasavyo usalama wa afya kazini,"amesema.
Amesema hali hiyo husababisha wafanyakazi kuwa katika hatari
ya kudhurika sehemu za kazi na kutokuwepo kwa mifumo au taratibu muafaka
za ndani za kushughulikia malalamiko.
Mapuri ameongeza kuwa jitihada za ukuaji wa viwanda unaweza
kuathiri haki za makundi mengine ambayo si wafanyakazi kama kuvunjwa kwa
haki ya kumiliki ardhi hasa kipindi cha utwaaji ardhi kwa ajili ya miradi
ya viwanda.
Amesema athari nyingine ni kukosa haki ya afya na mazingira
safi na salama endapo kuna uchafuzi kutoka viwandani na madhara ya ajira
kwa watoto kwani Tume imekuwa ikipokea malalamiko mengi ya uvunjwaji wa
haki za binadamu mahala pa kazi.
Ameongeza kuwa Serikali kama mdau wa maendeleo ya wananchi
itazingatia na kutekeleza jukumu la msingi la kulinda, kuheshimu na
kuzingatia haki za binadamu pale inapotekeleza miradi mbalimbali za
maendeleo.
Mkuu wa Idara ya Sheria Chama Cha Wafanyakazi wa Viwanda,
Biashara (TUICO), Noel Nchimbi amesema kumekuwa na malalamiko ya mahusiano
kati ya mwajiri na mwajiriwa huku akibainisha si kila mtu anapaswa
kuajiriwa.
"Ajira zipo nyingi, lakini si kila mtu anahaki ya kufanya kazi na kuajiriwa, mtoto chini ya miaka 14 hapaswi kuajiriwa kwani inaharibu afya zao hasa shuguli za migodini, mashambani na hata uvuvi ikibainika mwajiri atashitakiwa na kulipa faini ya sh milioni moja au kifungo mwaka mmoja au vyote kwa pamoja.
"Ajira zipo nyingi, lakini si kila mtu anahaki ya kufanya kazi na kuajiriwa, mtoto chini ya miaka 14 hapaswi kuajiriwa kwani inaharibu afya zao hasa shuguli za migodini, mashambani na hata uvuvi ikibainika mwajiri atashitakiwa na kulipa faini ya sh milioni moja au kifungo mwaka mmoja au vyote kwa pamoja.
Baadhi ya wafanyakazi hao wameitaka serikali kuangalia
mazingira bora na wezeshi kwa watu wenye ulemavu huku sheria za kazi
zizingatiwe kwa kila mfanyakazi.
Maadhimisho hayo yanalengo la kuikumbusha jamii umuhimu wa
kukuza na kulinda haki za binadamu katika Afrika na kuongeza uelewa wa
masuala ya haki za binadamu kama zinzvyotamkwa katika mkataba wa Afrika na
Haki za Binadamu na Serikali wa Afrika uliopitishwa June 1981.
No comments:
Post a Comment