HABARI NA MATUKIO PICHANI: ABBAS AIPONGEZA BOT KWA KUELIMISHA WAANDISHI WA HABARI
MKURUGENZI wa Idara
ya Habari MAELEZO, ambaye pia ndiye Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan
Abbasi, ameipongeza Benki Kuu ya Tanzania, (BoT), kwa kuandaa
semina ya mafunzo kwa waandishi wa habari za Uchumi na Fedha, iliyomalizika
mjini Unguja, Zanzibar leo Machi 31, 2017.
Dkt. Abaasi alisema, BoT,
kama taasisi ya serikali inao wajibu wa kuwapatia habari wananchi kupitia
waandishi wa habari na uamuzi wa kutoa mafunzo hayo ni ishara tosha ya
ushirikishaji wa waandishi katika kuhakikisha wananchi wanapatiwa habari sahihi
kutoka BoT.
“Tumekutana hapa wakati serikali
imepitisha sheria mbili, moja ni ile inayohusu huduma za vyombo vya habari, na
ya pili ni ile ya haki ya waandishi kupata taarifa kutoka taasisi za serikali
na mimi nikiwa kama msimamizi mkuu katika eneo hili la utoaji habari kwenye
taasisi za umma, ninawaalika mtusumbue sana katika kupata taarifa maana utoaji
wa habari kwa sasa si suala la utashi tena bali ni la kisheria.” Alisema
Dkt. Abbassi.
![]() |
| Dkt. Hassan Abbasi akizungumza wakati akiwasilisha mada juu ya Sheria mpya ya Huduma za vyombo vya Habari wakati wa kufunga semina ya mafunzo kwa waandishi wa habari za Uchumi na Fedha mjini Zanzibar |
![]() |
| Kaimu Meneja wa Uendeshaji wa Bot, tawi la Zanzibar, Bi.Graceana Bemeye, (aliyesimama), akitoa hotuba ya kufunga semina hiyo. Kulia ni Bi. Vicky Msina |
![]() |
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na
Msemaji Mkuu wa
Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, (Kushoto),
akipeana mikono na Mmiliki wa
K-VIS Blog, Bw. Khalfan Said mwishoni mwa
semina hiyo
|






No comments:
Post a Comment