Mbio za uchaguzi mkuu na vituko vya wanasiasa nchini Kenya: hebu fuatilia hii: halafu tuambie imeekaaje?
Mwanadada mmoja ambaye alikuwa mpenzi wa mbunge wa Kaunti ya Uasin Gishu nchini Kenya amefanya sherehe ya ‘kukata na shoka’ baada ya mwenza wake huyo kupigwa chini katika kinyang’anyiro cha kuwania tena kiti chake kuelekea uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya cha JP (Jubilee Party).
Mbunge huyo ambaye katika maisha ya mapenzi na mwanadada huyo walibarikiwa kupata watoto wawili, inasemekana ‘alim’mwaga’ mzazi mwenziwe mara tut u baada ya kukikwaa kiti hicho katika Uchaguzi Mkuu uliopita wa mwaka 2013 hivyo kumuacha mrembo na mzigo wa kuwalea watoto bila usaidizi wa ‘bwana mheshimiwa’ licha ya uwezo mkubwa alioupata kutokana na nafasi yake.
Matokeo hayo ya awali yanayomuweka ‘bench’ bwana huyo yamefufua matumaini kwa mwenza wake ambae licha ya ‘kusherehekea kwa nderemo na vifijo’ ameampa kumburuza mahakamani kudai matunzo kwa watoto…
- Star Ke.
No comments:
Post a Comment