BAD NEWS!! Kada mwengine wa CCM Wilayani Kibiti auawa kikatili akiwa nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo !


KIBITI: Mwenyekiti wa CCM tawi la Njia nne liliopo katika kijiji cha Muyuyu, kata ya Mtunda wilayani hapa ameuawa kwa kupigwa risasi usiku wa kuamkia leo akiwa nyumbani kwake.

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Juma Njwayo, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rufiji.. amemtaja  Mwenyekiti huyo aliyefariki dunia kuwa ni Iddy Seif Kirungi ambapo mwanae nae alijeruhiwa vibaya kwa kupigwa risasi tumboni. Alimtaja majeruhi kwa jina la Nurdin Iddy Kirungi.

Alisema marehemu alipigwa risasi akiwa kwake wakati akijaribu kukimbia.
Njwayo alisema kabla ya kuuwawa kwa Mwenyekiti huyo pia wauaji hao walianza kumjeruhi kwa kumpiga risasi tumboni mtoto wa marehemu ambayo ilimjeruhi vibaya na kukimbizwa Hospitali.

Mganga wa zamu katika kituo cha afya Ikwiriri, Dr Rashid Omar alisema walimpokea Nurdin akiwa na jeraha kubwa tumboni mwake ambalo halikutokeza upande wa pili.
Alisema majeruhi huyo walimpatia rufaa kwenda Hospital ya Mchukwi kutokana na kuwa anavuja damu nyingi sana...


...endelea kubofya: www.tanzaniampyamatukio.blogspot.com kwa habari mpya kila tunavyozipokea.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search