Dunia yaadhimisha siku ya Uhuru wa vyombo vya habari!

MEI 3 ya kila mwaka imetengwa maalumu na Umoja wa Mataifa (UN) kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani.

Siku hii iliidhinishwa kwa mara ya kwanza na umoja huo mwaka 1993 kutokana na mabadiliko makubwa ya kisiasa na uchumi duniani.


Waziri Mwakyembe
Lengo la siku hii ni kuangalia changamoto zinazokabili waandishi na mazingira wanayofanya kazi kama yanaridhisha au la,na kutambua pia mchango wa waandishi waliopigania taalamu ya uandishi wa habari hadi tone la mwisho la maisha yao.

Kwa lugha nyingine ni siku muhimu kwa waandishi wa habari kutathmini na kupitia changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo duniani. Hata hivyo, wakati siku hii ikidhimishwa jambo la kusikitisha ni kuwa vyombo vya habari vinafanya kazi katika kipindi kigumu hususan Afrika.
Sababu kubwa ni kwamba viongozi wengi wanaviona vyombo hivyo kama adui wao wakati kwa vile tu vinasema mambo ya ukweli. Ndiyo maana waandishi wanakamatwa, kushtakiwa na wakati mwingine maisha yao kuwa hatarini kutokana na kazi wanayofanya.

Ripoti ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani ya mwaka huu (2017) imeeleza mengi kuhusu hali halisi ya vyombo hivyo ilivyo duniani. Kwa mujibu wa ripoti hiyo Namibia, Ghana na Cape Verde ndiyo zinazotoa uhuru mkubwa kwa vyombo vya habari kwa upande wa Afrika. Hii maana yake kinachoendelea katika mataifa mengine ya Afrika ni ukandamizaji wa uhuru wa habari. Hii si habari njema hata kidogo.

Matokeo yake ni kwamba viongozi hawataki kuambiwa ukweli hata kama wanaongoza nje ya misingi ya utawala bora na sheria.
·         Nchi ambazo hazizingatii misingi hiyo kusema kweli maendeleo huwa duni na ujenzi wa utawala wa kidemokrasia hukosa mwenyewe.
·         Amani ndani ya nchi na mtu mmoja mmoja hufifia na watu kuishi kwa hofu kwa sababu tu ya kuwa na viongozi ambao si rafiki wa vyombo hivyo.
·         Ni katika mazingira hayo vyombo vya habari vinafanya kazi kwa kuchechemea na wakati mwingine vingine kukuta vikifungwa.
·         Si hivyo tu bali ni Afrika hii viongozi hutumia nguvu kubwa kutengeneza sheria kali ili vishindwe kufanyakazi kwa uhuru unaotakiwa.
·         Viongozi wanasahau kuwa bila uhuru wa vyombo vya habari hakuna maendeleo endelevu kwani mambo mengi hufanyika gizani.
·         Nchi zinazobana uhuru wa waandishi huishia kutumia nguvu nyingi katika mambo yasiyostahili na uonevu hutawala.
Ni kwa nini tunashindwa kujifunza kutoka nchi nyingine namna zinavyotoa uhuru mpana kwa vyombo vya habari na hakuna kinachoharibika?

Ripoti hiyo inasema Norway, Sweden, Finland zimeendelea kufanya vizuri katika kutoa uhuru wa vyombo hivyo pamoja na waandishi.

Ni lazima tukumbuke kuwa kukandamiza vyombo vya habari ni sawa na kuruhusu shetani kutamba altareni jambo ambalo si sahihi hata kidogo.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search