TAKUKURU wataja vinara wa Rushwa Temeke
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ‘TAKUKURU’
Mkoa wa Temeke imezitaja taasisi ambazo zinaongoza kwa kulalamikiwa kwa vitendo
vya rushwa ndani ya tisa iliyopita ikiongozwa na Halmashauri ya Temeke.
Akiongea na waandishi wa habari Mkuu wa TAKUKURU Mkoa
wa Temeke Pilly Mwakasege amezitaja taasisi hizo kuwa ni pamoja na Manispaa ya
Temeke, Mahakama, sekta binafsi, Polisi, Ardhi, Afya na Idara nyingine. Mpaka
sasa TAKUKURU imefungua mashauri mapya matatu Mahakamani huku mashauri manne
yakiwa yanaendelea kusikilizwa Mahakamani katika hatua mbalimbali huku ikiokoa
zaidi ya Tsh. 99m ikiwemo mishahara hewa na kujilipa posho isiyo halali ndani
ya miezi hiyo tisa.
Bofya hapa kumsikiliza kamanda mkuu wa TAKUKURU kanda ya Temeke:-blessnewstz



No comments:
Post a Comment