MORNING TALK: Rais JPM yuko ziarani Chato, fuatilia live yanayojiri.. Majaliwa akaribisha wawekezaji.. Rais Kenyatta aivimbia Mahakama.. #share.. TRA wafunguka kuhusu ukaguzi wa Risiti..



Fuatilia live ziara ya Mhe. rais Mjini Chato.

========= == =====   =====  =====
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewahakikishia uwekezaji wenye tija wawekezaji watakaokuja nchini kwa kuwa Tanzania ni nchi yenye amani, utulivu wa kisiasa na uchumi wenye kukua kwa kasi.


Ameyasema hayo jana (Jumapili, Julai 09, 2017) alipomuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli katika maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Aga Khan alipochaguliwa kuwa Imamu Mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani.
Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua na kuthamini shughuli mbalimbali zinazofanywa na mtandao wa taasisi za Aga Khan zilizopo hapa nchini, hivyo Serikali itaendelea kushirikiana nao.
Ameupongeza mtandao wa taasisi za Aga Khan kwa kumuunga mkono Rais Dkt. Magufuli katika kutoa kipaumbele cha kuwapa fursa watu wenye kipato cha chini kushiriki katika uzalishaji ili waweze kujikwamua kiuchumi.
"Nawahakikishia kwamba uwekezaji wenu hapa nchini utakuwa na baraka  kwa sababu nchi imetulia kisiasa na uchumi wake unakua kwa kasi. Nawaomba muendelee kuwaalika wanajumuia wa  madhehebu ya Shia Ismailia popote walipo duniani waje kuwekeza nchini fursa bado zipo."
Kwa upande wake Rais wa Jumuiya ya Madhehebu ya Shia Ismailia Tanzania, Bw. Amin Lakhani ameishukuru Serikali kwa ushirikiano inaowapa na kwamba ameahidi kuendelea kushirikiana nayo katika kuboresha sekta mbalimbali nchini.
Amesema mtandao wa maendeleo wa Aga Khan unatoa huduma mbalimbali zikiwemo za afya, elimu, kilimo na kunaendesha miradi katika mabara ya Afrika na Asia kwa kuwapa fursa watu wenye kipato cha chini kushiriki katika uzalishaji ili kujikwamua kiuchumi.

Awali, Mkuu wa wilaya ya Ilala, Bi. Sophia Mjema aliipongeza taasisi hiyo kwa mpango wake wa  upanuzi wa hospitali na kuongeza vituo 35 vya afya kutoka 15 walivyonavyo - EATV

================ ====  ================

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameonya mahakama nchini humo akiitaka kutousaidia upinzani na kuhujumu uchaguzi unaokuja.

Uchaguzi wa urais utafanyika mwezi ujao ambapo uhuru Kenyatta anataka kuchaguliwa tena.
Siku ya Ijumaa, kufuatia kesi iliyowasilishwa mahakamani na upinzani, mahakama kuu iliamrisha tume ya uchaguzi isichapishe makaratasi ya kupigia kura.
Bwana Kenyatta alisisitiza kuwa uchaguzi huo utafanyika jinsi ulivyopangwa.
Amesema kuwa mahakama hauwezi kudai kuwa huru na kutumia uhuru huo kuingilia idara zingine za serikali.
Muungano wa upinzani wa Nasa ulidai kuwa rais alikuwa na uhusiano na kampuni ya Dubai la Al Ghurair ambayo ilishinda zabuni ya dola milioni 24 kuchapisha makatasi hayo.
Hata hivyo Jaji mkuu wa Kenya David Maraga, ametoa onyo kwa Rais Uhuru Kenyatta kutohujumu imani ya umma juu ya mfumo wa kisheria.
Nayo tume ya Uchaguzi nchini Kenya IEBC leo inatarajiwa kukutana na wagombea wote wanane wa kiti cha uraisi akiwemo Rais Uhuru Kenyata.
Mawakili wa Tume hiyo pia watafika mbele ya mahakama ya rufaa kupata ufafanuzi zaidi juu ya uamuzi huo - Bongo5
==========  ============  =======

















About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search