Polisi wasema upelelezi kesi ya Lowasa haujakamilika # Atakiwa kurudi Julai 20... #share

Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Edward Lowassa ametakiwa kuripoti tena Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Alhamisi ya juma lijalo kutokana na upelelezi kutokamilika.

 
Lowassa alifika ofisi ya DCI kama alivyotakiwa kuripoti na baada ya kukaa nusu saa ndani alitoka na kuruhusiwa kuendelea na shughuli zake kutokana na upelelezi wa kosa linalomkabili la kutoa kauli za kichochezi kutokamilika.

Mwanasheria wa Lowassa, Peter Kibatala amewaambia wanahabari kuwa wamearifiwa na DCI kwamba upelelezi wa tuhuma hizo bado haujakamilika.

"Lowassa kama alivyoambiwa na uongozi wa jeshi la polisi ofisi ya DCI maelekezo ni kwamba turudi au arudi tena Alhamisi ya Julai 20 mwaka huu saa 3:00 asubuhi. Tutarudi tupate maelekezo zaidi', amesema Kibatala.

Lowassa aliingia matatani baada ya kuhoji hatua ya serikali kuendelea kuwashikilia masheikh wa kundi la uamsho bila ya kuwafikisha mahakamani kwa zaidi ya miaka minne huku akitaka kama hawana mashtaka waachiwe.

Tangu atoe kauli hiyo wakati wa futari ya mwezi wa ramadhan aliingia matatani na kutakiwa kufika ofisi ya DCI kwa ajili ya mahojiano na hadi sasa amekwishafika hapo mara tatu.
NA MWANDISHI WETU


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search