Utoro Temeke: Kamanda Gilles awahesabia siku waalimu... ataka wampe ripoti kamili.. #share

KAMANDA wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke,Gilles Muroto amewapa siku chache waalimu wa Mkoa huo wa kipolisi kurejesha marejesho juu ya ufatiliaji wa wanafunzi watoro shuleni.


Akizungumza leo katika Dae es Salaam katika Mkutano uliowakutanisha waalimu wa Mkoa wa Kipolisi Temeke amesema kila mwalimu anawajibu wa kujua maendeleo ya wanafunzi wake pindi wanapokuwa na maadhurio mazuri shuleni.

"Wajibu wa wazazi,walezi na waalimu kujua kwa kutambua mwenendo wa mwanafunzi kwanini maudhurio yake mabaya au kushuka kiwango chake cha ufaulu,"alisema Muroto.

Amesema oparesheni yetu ya kukamata wazazi itasaidia kupungunza utoro wa wanafunzi kwa sababu wazazi wakiea wakali wanafunzi watakuwa na maudhurio mazuri na watajiepusha kujiingiza katika makundi ya uhalifu.

Aidha amewata waalimu kufatilia mwenendo wa wanafunzi watoro ili kuweza kuwakamata wao pamoja na wazazi wao.

Amesema wanafunzi kumi na 16 waliokuwa eanashikiliwa na Jeshi hilo wamekwisha achiwa na kurudi shuleni huku wazazi 10 wao kupandishwa mahakama kwa kukiuka sheria ya mtoto.
Dalila Sharif.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search