GUMZO: Hali ya Afya ya Mbunge Esther Bulaya yazorota akiwa rumande,.. achomolewa na kulazwa Hospitalini.. #share

Baada ya kuingia 'matatani' na kutiwa rumande, Mbunge wa Bunda mjini Esther Bulaya amelazimika kutolewa kwa muda na kukimbizwa na kulazwa katika Hospital moja ya Mjini wa Tarime kutokana hali yake ya afya kubadilika akiwa katika kituo kikuu cha polisi alipokuwa amezuiliwa.


Mwenyekiti cha Chadema Wilaya ya Tarime Lucas Ngoto amesema Bulaya amelazwa kutokana na matatizo ya Kifua kubana.

"Mheshimiwa Bulaya anamatatizo ya kifua kubana hivyo hali yake ilibadilika kutokana na hali ya kule  rumande na Saa moja usiku huu akawa amepelekwa hospitalini na kulazwa wodi namba nane," amesema Ngoto.

Bulaya alikamatwa Jana jumamosi saa tisa  alasiri na jeshi la polisi Wilayani Tarime mkoani Mara na kuhojiwa kwa zaidi ya saa matatu kabla ya kupeleka Rumande ambapo hali yake ya afya imeanza kuzorota.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search