Gumzo: "Vijana wengi wa Kitanzania wamepata ujuzi, lakini wamekosa sifa za kuajiriwa.." ILO & VETA wametuletea course ya Uanagenzi.. #share
SHIRIKA la Kazi Duniani (ILO) limesema vijana wanaohitimu
Vyuo vya Mafunzo ya Ufundi Stadi na Vyuo Vikuu nchini wanakabiliwa na
changamoto ya ukosefu wa ajira kutokana kukosa sifa zinazohitajika kwenye soko
la ajira.
Aidha, limebainisha katika kukabiliana na changamoto hiyo limeanzisha Mradi wa Uanagenzi wenye lengo la kuwasaidia vijana wenye ujuzi ambao hawakupata fursa ya kupata elimu kwa kuwapeleka Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini (VETA) na Chuo cha Taifa cha Utalii ili waajiriwe katika sekta hizo.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Ofisa Miradi na
Uendelezaji wa shirika hilo Komoro Mwenda wakati akiwasilisha mada katika Siku
ya Pili ya Mkutano wa Kitaifa wa Vijana wa Afya na Maendeleo.
Amesema kumekuwapo na kundi kubwa la vijana linalohitimu
katika taasisi hizo huku akikisisisitiza kwa kiasi kikubwa ujuzi wanaopewa
haukidhi sifa wanazohitaji waajiri kusababisha ugumu wa upatikanaji ajira.
“ Ngazi ya vyuo vya ufundi na vyuo vikuu kuna idadi kubwa ya
vijana wamehitimu wana sifa lakini wanashindwa kuendana na mahitaji ya soko ya
ajira ndio maana wengi wao wanakosa ajira,” alisema Mwenda.
Mwenda amesema tayari ILO kwa kushirikiana na Serikali
limeanza kuwapeleka vijana kwenye vyuo hivyo kuwaongezea ujuzi na kuwasaidia
kutambulika kwenye fursa za ajira.
Amesesma mradi huo umelenga kuwasaidia vijana
wenye ujuzi wasiokuwa na vyeti vya taaluma waliohtimu elimu ya darasa la saba
na Kidato cha nne waliopata alama D katika masomo yao.
Ameongeza kuwa tatizo la ajira kwa vijana huwasabishia msongo
wa mawazo ambao huchangia kujiingiza katika matendo maovu yanayopoteza nguvu
kazi ya kazi ya taifa.
Kwa upande wa Makamu wa Rais wa Shirika la Kimataifa la Save
the Children Robert Clay amesema makundi ya vijana yanakabiliwa na changamoto
ya upangaji wa mipango kazi wa miradi ya maendeleo inayowahusu huku akiwataka
kuongeza jitihada kufanikisha hilo.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti na Kupambana na
Ukimwi nchini (TACAIDS), Jumanne Issango amesema utandawazi huchangia
mmomonyoko wa maadili sababu ya vijana kushindwa kuamua mambo wanaotakiwa
kuyafuata na wasiotakiwa kuyaiga.
Mwakilishi Mkazi wa Masuala ya Uzazi na Uzazi wa Mpango
nchini, Lulu Mwanakilala ameitaka jamii kuendelea kutumia njia za uzazi wa
mpango na kwamba kabla muhusika hajaanza kutumia huambiwa madhara ya njia hizo
na wataalamu.
Na Hussein Ndubikile
No comments:
Post a Comment