'MACHINGA'wapewa siku 3 kwa hiari yao kupisha mradi ujenzi wa barabara za juu (flyover) Ubungo mataa...#share

WAFANYABIASHARA wadogowadogo maarufu ‘Machinga’ wamepewa siku tatu kuondoka eneo la Ubungo mataa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam ili kupisha mradi wa ujenzi wa barabara za juu (Flyover) unaotarajiwa kuanza Septemba 3 mwishoni mwa wiki hii.

Kushoto ni Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Boniface Jacob na kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo John Kayombo wakizungumza na wafanyabiashara 'Machinga' leo Ubungo jijini Dar es Salaam


Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo John Kayombo akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuzungumza na wafanyabiashara hao juu ya kuondoka katika eneo hilo, alisema watatakiwa kuhama kuanzia jumamosi mchana kwenda katika soko la mwasiliano (Simu 2000).

“Maagizo ambayo tumekuja kuyatoa hapa kwa wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama ‘Machinga’ ni kuja kuzungumza nao kistaarabu kuwaomba sasa wapishe eneo la mradi wa Ubungo flyover,” alisema Kayombo.

Aidha alisema wakandarasi anataka kuanza ujenzi wa mradi huo na taratibu tayari zimekwisha kamilika kwani walishindwa kuanza kazi kutokana na kwamba Machinga walikuwa katika eneo la mradi.

Alibainisha kwa kuwa wamekwisha zungumza nao wamekubali kupisha eneo kwa hiari yao kutokana na faida za mradi huo huku akieleza kuwaonesha eneo zima la ujenzi unapoishia ili watakaopenda kuendelea kukaa kando ya barabara wajue pakuweka bidhaa zao nje ya mradi unapoishia.

Meya wa Manispaa hiyo Boniface Jacob alisema kuwa mradi huo ulitakiwa kuaza tangu Maei 22 mwaka ambapo wakandarasi waliopewa mradi huo wanazaidi ya siku 100 wakati mradi mzima ulitakiwa kukamilika ndani ya siku 980 hivyo siku zilizobaki ni takribani 818.

Alibainisha kuwa alifanya jitihada za kuzungumza na serikali paomoja na Tanroad ili kuhakikisha wafanyabiashara hao wanaondolewa kitarabu kwani kungetumika mabavu hata thamani ya mradi wenyewe ingeshuka.

Aidha alisema kuwa kupitia ofisi ya Mkurugenzi kumeandaliwa utaratibu mzuri utakaotumika kuwahamishia katika soko la mawasiliano na kueleza kuwa waliolengwa ni zaidi ya wafanyabiashara 2000.

Alisema watapewa stika maalumu zitakazowatambulisha na kupatiwa maeneo ya kufanyia biashara zao na kwamba hawataruhusu wasiohusika kupatiwa eneo.

Pia alisema kutokana na mradi huo kumetoakea fursa za ajira zaidi ya 1000 pamoja na mamantilie kupatia maeneo maalumu ambayo watajengewa vizimba kwa ajili ya kutoa huduma ya chakula kwa wafanyakazi ambao watakuwa katika shughuli za ujenzi wa barabara hiyo.














Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search