LHRC IMEZINDUA RIPOTI KUHUSU HAKI YA KUFANYA KAZI NA BIASHARA NCHINI ILIYOSHEHENI UKIUKWAJI ...#share

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimezindua Taarifa ya  Haki za Binadamu na Biashara ya mwaka 2016 huku kikibainisha taarifa hiyo imesheheni ukiukwaji mkubwa wa haki hizo kwenye masuala ya haki ya kufanya kazi, umiliki wa ardhi, usawa wa kijinsia, pamoja na kampuni kukiuka haki za binadamu.


Akizindua taarifa hiyo leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho Dk. Hellen Kijo Bisimba alisema tafiti ilifanyika katika mikoa 14 huku akibainsha inaonyesha asilimia 62.18 ya wafanyakazi hawana mikabata,  asilimia 61.60 hawana nakala za mikataba huku asilimia 38.40 pekee wakiwa nayo ikiwa imeandikwa.

“ Ripoti inabainisha wafanyakazi wengi hawana mikataba ya ajira wengi wao wanafanya kazi bila kupata haki ya msingi ikiwemo ya kunyimwa kupewa nakala za mikabata yao,’’ alisema Dk. Bisimba.

Dk. Kijo amesema imebainika makampuni hayapeleki michango ya wafanyakazi kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kwa mujibu wa sheria za kazi na kwamba  asilimia 45.85 wanalipwa muda wa ziada huku asilimia 54.15 wakinyimwa stahiki hiyo.

Amesisitiza kuwa wafanyakzi waliohojiwa na watafiti wa LHRC walibainisha kuwa asilimia 53.01 hakuna matawi ya vyama vya kutetea wafanyakazi makazini  ila asilimia 35.81 walisema vyama hivyo havina uwezo wa kuwakilisha vyema.

Ameoongeza kuwa katika suala la umiliki wa ardhi  tafiti zinaonyesha asilimia 50 ya ardhi inayomilikwa na wawekezaji haijaendelezwa na kwamba  vijiji vingi havina mpango madhubuti wa matumizi wa rasilimali hiyo.

Amefafanua kuwa  takwimu zinabainisha wanawake hawana kipaumbele cha kuapata ajira kwenye makampuni ukilinagnisha na wanaume ambapo asilimia 12.3 hawana ajira huku wanaume ikiwa asilimia 8.5 wana changamoto hiyo.

Pia alisema sekta ya viwanda imeonekana kuwapendelea zaidi wanaume  kwa asilimia 71.92 na wanawake ni asilimia 28.08 ya waliohojiwa wakiwa katika kazi.

Aidha, amesema kundi la watoto limeonekana kuingizwa kwenye ajira za utotoni kinyume na sheria za nchi ambapo asilimia 70 ya watoto walibainika kufanya kazi kwenye mashamba.

Katika hatua nyingine, amesema ripoti hiyo inaonyesha ukusanyayaji wa mapato ya ndani kwa mwaka umeongezeka hadi kufikia Sh trillioni 10.87 mwezi Julai wa mwaka huo.
Dk Kijo alisema makampuni yalionyesha uwajibikaji kwa jamii  kwa kushiriki uchangiaji wa madawati katika sekta ya elimu nchini.


Wakati huo huo, Dk Kijo amesema mwezi Juni mwaka jana wafanyakazi 2,464,399 walisajiliwa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii ukilinganisha na mwaka 2015 walisajiliwa  2,142,350.

Na Hussein Ndubikile

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search