mAHAKAMANI kISUTU: Video QueeN Agnes 'Masogange' azidi kubanwa matumizi dawa za kulevya...Mkemia Mkuu wa Serikali aushtukia mkojo wake kuwa na chembechembe ya dawa hizo...#share
OFISI ya Mkemia Mkuu wa Serikali imewasilisha katika Mahakama
ya Hakimu Mkazi Kisutu taarifa inayoonesha kuwa sampuli ya mkojo wa Video
Queen, Agnes Gerald "Masogange" una chembechembe za dawa za kulevya.
Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri amesema leo kwamba
pingamizi la upande wa utetezi kuwa fomu zilizopelekwa kwa mkemia hazikufata
sheria limetupiliwa mbali na mahakama imepokea taarifa hiyo ambayo itatumika
kama ushahidi.
Amesema shahidi wa kwanza ambaye ni Elia Mulima anahaki ya
kuandaa ripoti, kupima sampuli na kutoa ripoti mahakamani. Pia amesema Polisi
walipeleka maombi kwa mkemia wa serikali na kwamba ni wazi mshitakiwa alienda
kwa mkemia na askari wawili na kumpatia kontena kwa ajili ya kuweka sampuli ya
mkojo.
Mpelelezi kutoka Ofisi ya Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es
Salaam, WP Judith ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuwa alishuhudia
Masogange akitoa sampuli ya mkojo kwa kuwa alisimama mlangoni.
Amedai kuwa alipewa chupa ya plastiki yenye namba ya maabara
446/2017 na kumuelekeza Masogange jinsi ya kufanya ambapo alipata sampuli ya
mkojo huo.
Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula, shahidi huyo
alidai kuwa Februari 15, mwaka huu aliitwa na Kaimu Mkuu wa Upelelezi, Ramadhan
Kingai amchukue mshitakiwa Masogange na kumpeleka kwa Mkemia wa Serikali.
Amedai baada ya kuchukua aliongozana na Askari Polisi,
Sospeter kwenda kwa mkemia na kwamba saa 7 mchana walifika. "Lengo la
kumpeleka kwa mkemia ni kupimwa sampuli ya mkojo kwa kuwa alituhumiwa kwa
kutumia au kusafirisha dawa za kulevya," alidai Judith.
Hata hivyo, Wakili wa utetezi, Reuben Simwanza alimtaka shahidi huyo kueleza alikabidhiwa na nani chupa na kwamba mkojo ulikuwa na rangi ambapo shahidi huyo alieleza kuwa ulikuwa na rangi ya njano mpauko. Hakimu Wilbard Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 31, mwaka huu kwa ajili ya kusikilizwa.
Hata hivyo, Wakili wa utetezi, Reuben Simwanza alimtaka shahidi huyo kueleza alikabidhiwa na nani chupa na kwamba mkojo ulikuwa na rangi ambapo shahidi huyo alieleza kuwa ulikuwa na rangi ya njano mpauko. Hakimu Wilbard Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 31, mwaka huu kwa ajili ya kusikilizwa.
Na Mwandishi Wetu
No comments:
Post a Comment