gOOD nEWS: Mbunge wa Bunda Ester Bulaya atoka Hospitali Muhimbili alipokuwa amelazwa...#share
Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (Chadema) ameruhusiwa
kutoka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa takribani
wiki moja.
Bulaya alikimbizwa Muhimbili kutoka tarime mkoani Mara baada
ya kupata tatizo la kupumua baada ya kuzidiwa akiwa mahabusu ya kituo cha
polisi mjini Tarime. Alikuwa amelazwa wodi namba 18 katika jengo la Sewahaji
akipatiwa matibabu.
Mbunge huyo wa Chadema, leo Agosti 28 ameruhusiwa kutoka
hospitali na amewashukuru madaktari wa Muhimbili kwa kumpatia matibabu ya kina.
Amesema afya yake imetengemaa lakini amepewa maelekezo
kadhaa.
“Kwanza nitapumzika kwa siku 10, hivyo ndivyo nilivyoagizwa
na nitatakiwa kurudi tena hospitalini kwa ajili ya kuangaliwa afya yangu zaidi.
Kwa sasa nitapumzika kabla ya kurudi jimboni kuendelea na shughuli za
maendeleo,” amesema Bulaya.
Bulaya aliwekwa rumande Agosti 18 baada ya kukamatwa na
polisi akidaiwa kuingia jimbo la Tarime kufanya shughuli za kisiasa kwa kutoa
msaada wa mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu katika shule
za msingi kwa mwaliko wa mbunge mwenzake Esther Matiko.
Mwananchi:
Mwananchi:
No comments:
Post a Comment