Zitto asikitishwa na Anguko la mauzo ya bidhaa nje, adai hali hiyo kutufanya Tegemezi...#share

MBUNGE wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa   Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe, amesema kuwa mauzo ya bidhaa nje ya nchi hususan chakula yanazidi kushuka huku uingizaji wa bidhaa hizo kutoka nje ukipanda hasa kipindi hiki nchi inapopambana na ukuaji wa uchumi wa viwanda.

Zitto amesema hayo kupitia ukurasa wake wa facebook na Amebainisha kwa kusema kuwa anguko hilo, linatufanya  nchi kuzidi kuwa tegemezi.

“Uagizaji wa bidhaa za chakula kutoka nje umeongezeka kwa 14% ndani ya mwaka mmoja wa Mei 2016 mpaka Mei 2017, ambapo Tanzania ilitumia dola 480 milioni kuagiza vyakula kama sukari, nafaka na mafuta ya mawese. Tumekuwa tegemezi zaidi, tunauza bidhaa kidogo zaidi nje ya nchi, na tunanunua bidhaa zaidi kutoka nje", amesema
Zitto Kabwe.

Mbunge huyo amendelea kusema kuwa fedha ambayo serikali inapoteza kwa anguko la mauzo ya bidhaa ndani ya miaka miwili ni nyingi, ambayo ingeweza kununua ndege 23 za aina ya bomberdier Q400.


“Wakati Serikali inaimba viwanda, mauzo ya bidhaa zitokanazo na viwanda kwenda nje ya nchi yetu yameshuka sana, mwaka unaoishia Mei, 2016 Tanzania iliuza nje bidhaa za viwanda za thamani ya dola 1.5 bilioni. Mwaka mmoja baadaye Tanzania imeuza nje bidhaa za viwanda za thamani ya dola 0.8 bilioni tu. Anguko la mauzo nje la takribani dola 700 milioni sawa na thamani ya Ndege 23 za Bombadier Q400", aliandika Zitto Kabwe
Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search