nEWS: Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora yalaani shambulio katika Ofisi za IMMMA Advocates....Yalitaka Jeshi la Polisi kuharakisha upelelezi wa tukio hio...Pia waitaka TLS kusitisha mgomo wa siku 2 kesho na kesho kutwa....#share

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imelaani kitendo cha kupigwa bomu  Jengo la Ofisi za Wanasheria wa IMMMA zilizoko Barabara ya Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam kilichotokea usiku wa kuamkia Agosti 26 mwaka huu.


Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya jengo hilo kuvamiwa na kulipuliwa na kitu chenye mshindo mkubwa kinachodhaniwa ni bomu na kusababisha uharibifu mkumbwa huku ikiripotiwa hakuna kitu kilichochukuliwa.

Taarifa iliyotumwa leo kwa vyombo vya habari na Mwenyekiti wa tume hiyo Bahame Nyanduga, amesemna THBUB imesikitishwa na kitendo hicho na kwamba kinaashiria uhalifu wenye nia ya kutisha wanasheria wasitekeleze majukumu yao ya kisheria ya kutetea wateja wao.

Nyanduga amesema tume hiyo inasisitiza kuwa dhana ya utawala bora inategemea utawala wa sheria, ambao utaathirika iwapo wanasheria watatishwa na matukio kama ya kupigwa mabomu au vitendo vinginevyo vitakavyowanyima uhuru wa kufanya kazi zao.

Amesisitiza kuwa tume inalitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha linakamilisha upelelezi wa tukio hilo na kuwapeleka wahusika katika vyombo vya sheria.

Aidha, ameutaka uongozi wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) kusitisha tamko lililowataka Mawakili kususia kuhudhuria Mahakamani na Mabaraza ya aina zote kwa siku mbili kwani mgomo huo hautakuwa na maana kwa kuwa vyombo vya usalama vimeshaanza kufanya uchunguzi.
Pia  amesema ni vyema TLS ikasitisha mgomo huo kwani utawaathiri wateja wao ambao hawahusiki na tukio la kupiga bomu.
Na Mwandishi Wetu


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search