nEWS: Serikali yawataka vijana kuacha kulalamika...Yawahimiza kuchangamkia fursa kujikwamua kiuchumi....#share

SERIKALI imwataka vijana kuacha tabia ya kulalamika badala yake wajikite katika kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo ili kujikwamua kiuchumi huku ikibainisha inaendelea na hatua za uanzishwaji wa Baraza la Vijana la Tanzania.


Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Bunge, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Jenista Mhagama wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Vijana wa Kitaifa wa Afya na Maendeleo.

Amesema vijana wengi wamejenga utamaduni wa kulalalmika hali ya ngumu ya maisha pasipo kutimiza wajibu wao kwa kuhangaikia fursa kuzifanyia kazi huku akisisitiza endapo watazifanyia kazi zitawasaidia kujikwamua kimaisha.

''Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea na jitihada za kuwasaidia vijana kinachotakiwa vijana waache kupiga kelele bila kutimiza wajibu wao fursa zipo nyingi zinazoweza kuwawezesha kiuchumi,'' alisema Jenista.

Waziri Jenista amesema vijana wanatakiwa kutumia akili zao kama mtaji kupambanua mambo na mazingira yanayowazunguka kujiletea maendeleo.

Amesisitiza kuwa Sheria namba 12 ya mwaka 2015 inayohusiana na uundwaji wa baraza hilo ilikwishatungwa kanuni huku akiongeza lengo la kuwa na chombo hicho ni kuwaleta vijana pamoja na Serikali yao.

Amefafanua kuwa katika kuhakikisha kundi hilo linajikwamua kiuchumi vijana 2,500 wameanza kupatiwa mafunzo katika kiwanda cha Tuki Garmert kilichopo Ubungo ya utengenezaji wa nguo zitakazouzwa nje ya nchi.

Pia amesema vijana 1,000 wanaendelea kupatiwa mafunzo ya uongezaji thamani wa bidhaa za ngozi huku 13,400 waliopo kazini wakipewa mafunzo hayo ambapo waemilishaji rika 60 watasambazwa mikoani kuwaelimisha vijana.

Amewashauri vijana kupima virusi vya Ukimwi kwa hiari katika vituo vinavyotoa huduma hiyo ili kutambua hali za afya zao.

Kwa upande wake MKurungenzi wa Shirika la Save the Childern nchini Peter Wash amesema mkutano huo utasaidia kupatikana kwa ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili vijana zikiwemo za ukosefu wa ajira, magonjwa na uchangamkiaji fursa.

Kaimu Mkurugenzi wa Tume ya Kuratibu na Kudhibiti Ukimwi nchini (TACAIDS) Jumanne Isango amewataka vijana kuendelea kufanya jitihada za kujiletea maendelea na kujikinga na maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwani kundi hilo linaongoza kwa maambukizi hayo.

Na Hussein Ndubikile

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search