sPORTS nEWS: Zama za ubabaishaji TFF sasa kwisha, Rais Karia aanza kwa kushusha rungu kali Bodi ya ligi kwa kuvurunda.....#share

KAIMU Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Alfred Kidao amesema kuwa ameagizwa na rais wa Shrikisho hilo, Wallace Karia kumwandikia barua Mtendaji mkuu wa Bodi ya Ligi ili kuwaadhibu viongozi wa Bodi ya Ligi waliohusika na kupanga ratiba.


Pichani ni Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi ni Boniface Wambura.

Kumekuwa na malalamiko kutokana na Bodi hiyo kupanga ratiba ya ligi ambapo walishindwa kuzingatia kuwa kuna michezo ya kimataifa ambayo itahusisha timu za taifa jambo ambalo limesababisha baada tu ya mchezo mmoja tu, ligi hiyo ikapanguliwa tena.


“Nimeagizwa na rais nimwandikie barua mtendaji mkuu wa bodi ya ligi ili aweze kuwachukulia hatua viongozi wa bodi hiyo waliohusika na kupanga ratiba hii pamoja na kwamba walikuwa na kalenda lakini bado wamekosea,” alisema Kidao.

Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi ni Boniface Wambura ambaye sasa atakuwa na jukumu la kuchukua hatua kwa wasaidizi wake.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search