tETESI zA uSAJILI uLAYA: Wakati dirisha la usajili likielekea kufungwa Wenger hamtaki Mustafi...Adumu na Arsenal kwa miezi 12..... Awekwa sokoni....#share

KLABU ya Arsenal huenda ikaachana na beki wake Shkodran Mustafi kabla ya dirisha la usajili la msimu huu wa kiangazi kufungwa Alhamisi ya wiki ijayo.

Kwa mujibu wa Daily Mail Online imearifu kuwa Arsene Wenger amefungua milango ya kumuuza mchezaji huyo amabaye amedumu na klabu hiyo kwa mwaka mmoja tangu aliposajiliwa msimu uliopita.

Aidha taarifa zinaeleza kuwa Juventus na Inter Milan wameonyesha kumhitaji mchezaji huyo. Klabu ya Inter Milan tayari imeshamuulizia mchezaji huyo huku Juventus pia wakiwa wakifuatilia kwa karibu uwezekano wa kumsajili.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujeruman alijiunga na Washika Mtutu hao wa London msimu uliopita wa kiangazi kwa pauni milioni 35 lakini kwa sasa klabu hiyo iko tayari kuachana naye.

Arsenal wanataka kurudisha kiasi hicho cha fedha walichotumia kumnunua Mustafi hivyo kiasi cha ada ambacho kitakaribiana na pauni milioni 35 kikitolewa na timu yoyote inayomhitaji klabu inaweza kumuuza.

Mustafi alionyesha kiwango kizuri katika miezi ya mwanzoni msimu uliopita, lakini kuelekea mwishoni mwa msimu huo kiwango chake kilianza kilishuka na ilisababishwa na kuwa majeruhi.

Na Mustafi siyo mchezaji pekee anayehusishwa kuihama   Emirates msimu huu wa kiangazi  lakini pia Alex Oxlade-Chamberlain huenda akaihama klabu hiyo. 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search