CWT Geita kimewatangaza Mashujaa wa Elimu, Wanafunzi walifariki kwa ajali Ziwa Victoria..
Na,Denice Simba
Chama cha walimu CWT tawi la Geita kimewatangaza wanafunzi watatu waliopoteza maisha katika ziwa Victoria wakati wakivuka kutoka shuleni kuwa mashujaa wa elimu
Wanafunzi hao wa Shule ya msingi Butwa walipoteza maisha katika ajali ya majini iliyotokea mwezi juni mwaka huu baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kupinduka na kuzama
Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake,Katibu wa CWT wilaya ya Geita Mwl. John Kafimbi amesema Chama chake kinafanya maandalizi ya kujenga makaburi ya wanafunzi hao kama sehemu ya makumbusho
Aidha, Mw. Kafimbi ameeleza kuwa vifo vya watoto vimekuwa chachu ya maboresho kat ka sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na mipango ya kujengwa shule mpya ya msingi katika kisiwa cha Butwa-Lulegea.
Chama cha walimu CWT tawi la Geita kimewatangaza wanafunzi watatu waliopoteza maisha katika ziwa Victoria wakati wakivuka kutoka shuleni kuwa mashujaa wa elimu
Wanafunzi hao wa Shule ya msingi Butwa walipoteza maisha katika ajali ya majini iliyotokea mwezi juni mwaka huu baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kupinduka na kuzama
Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake,Katibu wa CWT wilaya ya Geita Mwl. John Kafimbi amesema Chama chake kinafanya maandalizi ya kujenga makaburi ya wanafunzi hao kama sehemu ya makumbusho
Aidha, Mw. Kafimbi ameeleza kuwa vifo vya watoto vimekuwa chachu ya maboresho kat ka sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na mipango ya kujengwa shule mpya ya msingi katika kisiwa cha Butwa-Lulegea.
No comments:
Post a Comment