Mbunge Lazaro Nyalandu: Madaktari Nairobi Kalamu zao Nzito Kuandika Ripoti Mwenendo matibabu ya Lissu...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360..#share

MBUNGE  wa Jimbo la Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu amesema kwamba wamekuwa wakisubiri Madaktari watoe ripoti ya mwenendo wa matibabu ya Tundu Lissu ili kuwapatia Madaktari Bingwa wa Marekani.
Image result for lazaro nyalandu na Tundu lissu
Ameeleza hayo kupitia ukurasa wake wa Facebook na kudai kuwa ripoti hiyo ni kwa ajili ya kuona uwezekano wa Lissu kupatiwa rufaa kwa matibabu zaidi nje. Lakni amebainisha kuwa kalamu zao zimekuwa nzito kuandika kuiandika kwa siku tatu tangu waahidiwe.

Kupitia Ukurasa wake wa Facebook ameandika  “Tumekuwa #NairobiHospital tukisubiri MADAKTARI watoe RIPOTI ya mwenendo wa MATIBABU ya Mh #TunduLissu kwa minajili ya kuwapatia MADAKTARI BINGWA wa Marekani na kuona uwezekano wa Mh #TunduLissu kupatiwa RUFAA kwa matibabu zaidi NJE., LAKINI bado KALAMU zao ni nzito kuandika RIPOTI hii siku ya tatu tangu tuahidiwe,”.

“Binafsi, nimerudi NAIROBI tangu JANA kushiriki maandalizi ya uwezekano wa kumhamishia Mh TunduLissu Marekani kwa ajili ya huduma yenye ubora zaidi, endapo MADAKTARI wa #NairobiHospital wangeridhia. Kesho asubuhi nitarejea hospitalini kusikiliza kauli ya mwisho ya MADAKTARI kuhusu RIPOTI hiyo,” .


Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search