Mbunge Msigwa Ashangaa Takukuru Kushindwa Kuwahoji Mbunge Msukuma na RPC Geta..Ni Kutokana na Kauli Tata ya Msukuma Dhidi ya RPC..Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360

MBUNGE wa Iringa Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Peter Msigwa amezidi kushikilia suala la Mbuge wa Geita Mjini na RPC wa Geita na kusema kuna jambo kati yao lakini anashindwa kuelewa inakuaje mbaka sasa TAKUKURU inashindwa kuwahoji wote wawili.

Msigwa amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter zikiwa zimepita siku kadhaa toka Mbunge na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita, Joseph Msukuma kudai kuwa ana siri nyingi za Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Mponjoli Mwabulambo na kudai atazitoa siri hizo ikiwa Kamanda wa Polisi huyo hatamuomba msamaha kwa kitendo alichomfanyia ikiwa pamoja na kumkamata na kumlaza rumande.

"Msukuma amesema anajua siri za RPC wa Geita , TAKUKURU kwa nini hamjiongezi kuwahoji wote wawili, kuna kitu hakipo sawa kinaendelea hapa" ameandika Msigwa.


Mbunge wa Geita alikamatwa na jeshi la polisi na kulazwa rumande kwa masaa 24 kufuatia vurugu zilizofanywa katika mgodi wa Geita Gold Mine (GGM) lakini alipotoka Mbunge huyo alianza kumshtumu RPC wa Geita na kusema anafahamu mambo yake mengi, akahitaji kuombwa msamaha ndani ya siku tatu na RPC huyo huku akiahidi kutoa siri zake kama hatafanya hivyo.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search