Sued Kubenea Ashikiliwa Na Jeshi la Polisi...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360..#share

WAKATI serikali ikiwa imelifungia Gazeti la Mwanahalisi ambalo linamiliwa na Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea ,KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, polisi wenye silaha wamezingira hospitali  ya Agha Khan aliyokuwa ameenda kupata huduma ya matibabu, Mbunge Kubenea na kumsubiri atibiwe kisha kuondoka naye.

Taarifa zinasema polisi hao wameelekea kituo cha Oysterbay jijini Dar es Salaam ingawa haijajulikana wanapompeleka na kwa kosa gani.

Wiki iliyopita Spika Job Ndugai aliviagiza vyombo vya dola kuwakamata Kubenea pamoja na Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe na kuwafikisha mbele ya Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama.

Hii inatajwa kuwa Mbunge huyu anapitia naye katika kipindi kigumu kwenye  cha awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli tangia iangie madarakani amekumbana na misukosuko ya Biashara zake za Magazeti kutokana serikalii hii kuyafungia Magazeti yake yote.

Magazeti yake hayo ni Mawio,Mwanahalisi pamoja Mseto ambayo yamefungiwa kutokana na kuandika habari zinazodaiwa kuwa ni za uchochezi.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search