Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Asikitika Kuzuliwa Jambo Mitandaoni.... Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360.. #share

RAIS Msaafu wa Awamu ya Nne amezuliwa jambo katika mitandao ya kijamii. 

Katika hali ya kushangaza kumekuwa na ujumbe unaosambaa katika mtandao wa Facebook ukionyesha kunukuu maneno ya Rais Kikwete ambayo yanaonyesha kama kuipiga dongo Serikali.

Ujumbe huo unasema "Pale unapomuona mtu anajaribu kumlazimisha Mbwa asibweke wakati ni sehemu yake kubweka lazima utajiuliza huyu mtu utumia nini wakatio wakufikilia,"

"Lakini naomba mtambue kuwa unapokuwa kiongozi unapokuwa na busara na kuheshimu maoni ya watu wa pembeni yako utaqhishia kuwamaliza viongozi wenzako ukihisi ni maadaui," umesema ujumbe huo 

Kufuatia ujumbe huo Rais Kikwete amatoa neno kupitia ukurasa wake wa Twitter kukanusha suala hilo akisema,

"Nasikitishwa sana na uvumi huu unaosambazwa juu yangu.Inasikitisha sana. Inasikitisha zaidi kuwa wako watu timamu wanaoamini uzushi huu," ameandika Rais Kikwete.

Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search