Wasanii Nchini Washauriwa Kufanya Kazi na Taasisi za Kifedha...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360...#share

WASANII wa tasnia mbalimbali nchini wameshauriwa kufanya kazi kwa kuzitumia taasisi za kifedha ili waweze kupata fursa za mikopo, wafadhili na uingiaji mikataba itakayosaidia uendeshaji wa makundi yao.

 Katika picha wa katikati ni 0fisa Masoko wa Benki ya DTB, Ally Mbwana, Kushoto kwake  ni ofisa mwenzie, Lisa Mugerezi Na Kulia kwake ni Mtendaji Wa Basata, Rajab Solo wakizungumza katika jukwaa la sanaa jijini Dar es Salaam Leo.

Ushauri huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Afisa Masoko wa Benki ya Diamond Trust Bank (DTB), Ally Mbwana katika Jukwaa la Sanaa lililokuwa likijadili umuhimu wa wasanii kufanya kazi na taasisi hizo.

Amesesma wasanii wamekuwa wakishindwa kupiga hatua kutokana na kutoshrikiana na taasisi za fedha ikiwemo ufunguaji akaunti za makundi hali inayowasabishia kukosa mikopo na wafadhili wenye nia kuyaunia makundi hayo.

''Wasanii wafanye kazi kwa kuzitumia benki katika kuendesha makundi hata wafadhili  hawawezi kulisaidia kundi bila kuonyeshwa akaunti inayoeleweka,'' amesema Mbwana.

Amesisitiza kuwa makampuni mengi hayawezi kusaini mikataba na vikundi vya sanaa bili kuhakikisha kikundi kina mwongozo wa akaunti madhubuti.

Amewashauri wasanii kuchangamkia fursa za DTB kwa kufungua Akaunti Maalum kwa ajili ya vikundi vyao kwa gharama ya Sh 100,000 huku akibainisha akaunti itawasaidia kuhifadhi fedha zao na kulipia gharama za kodi ya majengo.
Kwa upande wake Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Rajab Solo ameipongeza benki hiyo kwa mipango madhubuti yenye lengo la kuwakomboa wasanii.

Naye Msanii wa maigizo, Mcdonald Hule ameiomba benki hiyo kufikiria mpango wa kuanza kutoa elimu ya mikopo itakayowasaidia kwenye ununuzi wa vifaa vya muziki na uimarishaji makundi.

Msanii Maraiam Mponda'Mama Mipango ameishukuru benki hiyo na kuiomba iendelee kuwasaidia kutoka mahala waliko na kutambulika kimataifa.
                                       
Na Hussein Ndubikile

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search