Hali ya Ajira Kwa Sasa Nchini Yazidi Kuwa Tete...Mgodi Huu Wapunguza Wafanyakazi...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360....#share
UNAWEZA ukasema sasa ajira nchini
inaendelea kuwa kizungumkuti kwa vijana wengi wa kitanzania. Hii ni kutokana na
Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia kupunguza
wafanyakazi 2,000 kutokana na mgodi kupunguza uzalishaji.
Hatua hiyo inatokana na mgodi huo kuingia mgogoro na Serikali
baada ya kuzuiwa kusafirisha makinikia kwenda nje ya nchi.
Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa Kampuni ya Acacia, Asa Mwaipopo
alisema hayo juzi wakati wa hafla ya kuwaaga wafanyakazi hao waliopunguzwa.
Mwaipopo alisema kati ya wafanyakazi 2,000 waliopunguzwa,
1,200 ni waajiriwa wa Bulyanhulu na 800 ni kutoka kwenye kampuni zenye zabuni
zinazofanya kazi katika mgodi huo.
Alisema kutokana na zuio la Serikali la kusafirisha mchanga
wa dhahabu (makinikia) nje ya nchi, mgodi huo umebadili mfumo wa utendaji kwa
kuanzisha mtambo mpya utakaochenjua mabaki ya awali kwa kutumia kemikali ya
Cyanide.
Meneja huyo alisema njia hiyo imeelezwa itatoa kiwango kidogo
cha dhahabu, tofauti na uchimbaji wa awali wa mtambo mkubwa uliokuwa ukizalisha
makinikia yenye dhahabu nyingi zaidi.
Hata hivyo, Acacia iliwahi kueleza kuwa kiwango cha dhahabu
kinachobaki kwenye makinikia ni kidogo.
Mwaipopo alisema katika mfumo mpya wa mtambo wa uzalishaji
kwa kutumia kemikali hiyo, wataajiri upya wafanyakazi 150 wa kampuni na wengine
150 kutoka kwenye kampuni zenye zabuni ambao watakuwa wakifanya usafi, ulinzi
na huduma ya chakula.
Alisema mtambo mkubwa uliokuwa ukitumika kwa uzalishaji
umekamilisha kazi Jumamosi, hivyo kufikia mwisho wa uzalishaji makinikia katika
mgodi huo.
Mwaipopo alisema licha ya mgodi kupunguza uzalishaji na
wafanyakazi, lakini ulipaji wa ushuru wa huduma kwa halmashauri na kodi za
Serikali utaendelea ingawa kwa kiwango kidogo.
Kuhusu wafanyakazi waliopunguzwa, Mwaipopo alisema licha ya
kuagana nao wamewapa mafunzo ya ujasiriamali na kuwaandaa kisaikolojia kwa
kuwafundisha namna ya kuishi maisha mbadala tofauti na waliyokuwa nayo wakati
wa ajira.
Vyama vya wafanyakazi
Mwakilishi wa vyama vya wafanyakazi katika mgodi huo,
Kazimili Lubigisa alisema Jumamosi ilikuwa siku maalumu ya kumuaga Meneja Mkuu
wa mgodi huo, Graham Crew lakini kwa masikitiko na hali ambayo haikutarajiwa
iliwageukia wafanyakazi wote.
Lubigisa alisema kufungwa kwa mtambo huo kumesababisha
madhara makubwa kwa wafanyakazi na Serikali kwa jumla, zikiwamo familia zao
ambazo zimeathirika kiuchumi, elimu, afya na kisaikolojia. Pia, alisema vijiji
14 vinavyozunguka mgodi vitaathirika kiuchumi, kielimu, kiafya, miundombinu ya
barabara na mapato ya Serikali.
Alisema makandarasi wanaofanya kazi katika mgodi huo nao
wameathirika, hivyo ameiomba Serikali kuharakisha mazungumzo ili kuepusha
madhara zaidi.
Akiwaaga wafanyakazi hao, Crew anayeondoka baada ya kufanya
kazi katika mgodi huo kwa miaka miwili, alisema hakuna anayefurahia hatua
iliyopo lakini akawataka kuendelea kuwa na imani kuwa mazungumzo yanayoendelea
baina ya uongozi na Serikali yataleta mwafaka.
Mwananchi:
UNAWEZA ukasema sasa ajira nchini
inaendelea kuwa kizungumkuti kwa vijana wengi wa kitanzania. Hii ni kutokana na
Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia kupunguza
wafanyakazi 2,000 kutokana na mgodi kupunguza uzalishaji.

Hatua hiyo inatokana na mgodi huo kuingia mgogoro na Serikali baada ya kuzuiwa kusafirisha makinikia kwenda nje ya nchi.
Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa Kampuni ya Acacia, Asa Mwaipopo
alisema hayo juzi wakati wa hafla ya kuwaaga wafanyakazi hao waliopunguzwa.
Mwaipopo alisema kati ya wafanyakazi 2,000 waliopunguzwa,
1,200 ni waajiriwa wa Bulyanhulu na 800 ni kutoka kwenye kampuni zenye zabuni
zinazofanya kazi katika mgodi huo.
Alisema kutokana na zuio la Serikali la kusafirisha mchanga
wa dhahabu (makinikia) nje ya nchi, mgodi huo umebadili mfumo wa utendaji kwa
kuanzisha mtambo mpya utakaochenjua mabaki ya awali kwa kutumia kemikali ya
Cyanide.
Meneja huyo alisema njia hiyo imeelezwa itatoa kiwango kidogo
cha dhahabu, tofauti na uchimbaji wa awali wa mtambo mkubwa uliokuwa ukizalisha
makinikia yenye dhahabu nyingi zaidi.
Hata hivyo, Acacia iliwahi kueleza kuwa kiwango cha dhahabu
kinachobaki kwenye makinikia ni kidogo.
Mwaipopo alisema katika mfumo mpya wa mtambo wa uzalishaji
kwa kutumia kemikali hiyo, wataajiri upya wafanyakazi 150 wa kampuni na wengine
150 kutoka kwenye kampuni zenye zabuni ambao watakuwa wakifanya usafi, ulinzi
na huduma ya chakula.
Alisema mtambo mkubwa uliokuwa ukitumika kwa uzalishaji
umekamilisha kazi Jumamosi, hivyo kufikia mwisho wa uzalishaji makinikia katika
mgodi huo.
Mwaipopo alisema licha ya mgodi kupunguza uzalishaji na
wafanyakazi, lakini ulipaji wa ushuru wa huduma kwa halmashauri na kodi za
Serikali utaendelea ingawa kwa kiwango kidogo.
Kuhusu wafanyakazi waliopunguzwa, Mwaipopo alisema licha ya
kuagana nao wamewapa mafunzo ya ujasiriamali na kuwaandaa kisaikolojia kwa
kuwafundisha namna ya kuishi maisha mbadala tofauti na waliyokuwa nayo wakati
wa ajira.
Vyama vya wafanyakazi
Mwakilishi wa vyama vya wafanyakazi katika mgodi huo,
Kazimili Lubigisa alisema Jumamosi ilikuwa siku maalumu ya kumuaga Meneja Mkuu
wa mgodi huo, Graham Crew lakini kwa masikitiko na hali ambayo haikutarajiwa
iliwageukia wafanyakazi wote.
Lubigisa alisema kufungwa kwa mtambo huo kumesababisha
madhara makubwa kwa wafanyakazi na Serikali kwa jumla, zikiwamo familia zao
ambazo zimeathirika kiuchumi, elimu, afya na kisaikolojia. Pia, alisema vijiji
14 vinavyozunguka mgodi vitaathirika kiuchumi, kielimu, kiafya, miundombinu ya
barabara na mapato ya Serikali.
Alisema makandarasi wanaofanya kazi katika mgodi huo nao
wameathirika, hivyo ameiomba Serikali kuharakisha mazungumzo ili kuepusha
madhara zaidi.
Akiwaaga wafanyakazi hao, Crew anayeondoka baada ya kufanya
kazi katika mgodi huo kwa miaka miwili, alisema hakuna anayefurahia hatua
iliyopo lakini akawataka kuendelea kuwa na imani kuwa mazungumzo yanayoendelea
baina ya uongozi na Serikali yataleta mwafaka.
Mwananchi:
No comments:
Post a Comment