Wizara ya Afya Yapokea Msaada wa Mashine ya Kutoa Dawa ya Usingizi...Soma Habari Kamili na Matukio360..#share

WIZARA  ya  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imepokea msaada kutoka kwa Muungano wa Utepe Mweupe wa Uzazi Salama (WRATZ) wa mashine ya kutoa dawa ya usingizi wakati wa upasuaji yenye thamani ya zaidi ya sh. milioni 60.

Akipokea msaada huo leo jijini Dar es Waziri wa Wizara hiyo Ummy Mwalimu, amesema mashine hiyo itasaidia kupunguza vifo vya watoto na akina mama wakati wa kujifungua.

“Kwa mujibu wa takwimu ni kwamba hivi sasa wanawake 30 hufariki kila siku, inamana kuwa kwa mwezi hufariki wanawake 900,” amesema Waziri Ummy.

Aidha Ummy amesema katika kuhakikisha wanaboresha mazingira ya huduma za afya kwa wazazi na watoto ni kwamba serikali imejipanga kabla ya mwezi Juni mwakani kuongeza vituo vya 170 vya kutoa huduma ya uzazi kote nchini.

Waziri Ummy ameongeza kuwa serikali imetenga sh.bilioni 8 kwa ajili ya kununulia vifaa pamoja na dawa kwa ajili ya kuboresha huduma za afya ili kukabiliana na vifo vya akina mama hao na watoto.

Kwa upende wake Mratibu wa Taifa wa WRATZ Rose Mlay, amesema lengo la msaada huo ni kwa sababu wameona kuwa wanao wajibu wa kusaidia kuokoa maisha ya wazazi na watoto wakati wa kujifungua.

“Mashine hii itatumika kunusuru maisha ya mama na mototo, lakini na watu wengine. Hili ni jambo la kujivunia,” amesema Mlay.

Akitoa ufafanuzi wa jinsi inavyofanya kazi mashine hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dk. Mpoki Ulisubisya amesema inauwezo wakutengeneza asilimia 21 ya hewa ya oksijeni kwa ajili ya kumsaidia mgonjwe.


Aidha amesema kuwa hata umeme unapokatika ina uwezo wakutumia hewwa ya oksijeni ya kawaida ambayo inatumiwa na watu wengine.

Dk. Ulisubisya amesema msaada huo ni hatua kubwa katika maendeleo ya uboreshwaji wa huduma za afya nchini, lakini amesema kuwa kinachotakiwa kwa sasa ni kuandaa wataalamu wakutumia mashine za jinsi hiyo.


Mashine ya kutoa usingizi wa kati wa huduma ya upasuaji msaada uliotolewa kwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto leo jijini Dar es Salaam na WRATZ

Na Abraham Ntambara



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search